Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Friday, July 22, 2011

Maana sahihi ya neno 'fisadi'

Leo hii wakati nikisikiliza kipindi cha Kipima Joto cha ITV kinachoongozwa na Rainfred Masako, nimemsikia Profesa Tigiti Sengo akitoa ufafanuzi kuhusu matumizi sahihi ya neno 'fisadi'. Alisema:
Fisidi ndiyo mwizi; fisadi ni malaya na mlevi.
Huyu ni gwiji wa lugha ya Kiswahili. Natabiri kuwa miaka 20 tangu leo hii, Watanzania wataendelea kutumia neno ‘fisadi’ kama ambavyo linavyotumika sasa hivi kwa makosa. Au inawezekana mafisidi hawatakuwepo wakati huo.

No comments: