Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Sunday, May 13, 2012

Timu ya waTanzania DMV yatoka sare na Ethiopia B

Timu ya waTanzania DMV imetoka sare, bila kufungana, na timu ya Ethiopia B katika mchezo uliochezwa jana huko Burtonsville, Maryland, nchini Marekani katika ligi ya Diaspora World Cup.
Kikosi kamili cha timu ya waTanzania DMV wakiwa na mdhamini mpya wa timu hiyo, mbunifu wa mitindo ya Kwetu, Missy Temeke, akiwa na na shabiki Didi Vava, katika uwanja wa Greencastle, uliopo Burtonsville, Maryland.
Mchezaji wa timu ya Ethiopia akipambana vikali na Yousouf Godson Liuzinho, kipindi cha kwanza, katika ligi ya 2011 Diaspora World Cup kwenye kiwanja cha Greencastle, kilichopo Burtonsville, Maryland.
Wachezaji wa wa timu ya Ethiopia wakiwania freekick katika dakika ya 62 ya mchezo huo.
Didi Vava, kushoto, akiwa na Sharif Qullatein, Dogo Hudhaifa Shatry, na mmiliki wa blog ya swahilivilla Abou Shatry, wakiwa katika jukwaa la wapenzi wa timu ya waTanzania DMV.
Mdhamini wa timu ya waTanzania DMV ambaye ni mwanamitindo na mbunifu wa mitindo ya Kwetu Fashion Design, Missy Temeke, akiwa na Bendera ya Taifa.

Picha na habari kutoka kwa mwana blog Abou Shatry wa http://swahilivilla.blogspot.com/

No comments: