Mtanzania Ramadhani Shauri atapanda
ulingoni siku ya Idd pili kupambana na bondia Sande Kizito kutoka Uganda
kugombea mkanda wa IBF katika bara la
Africa katika uzito wa unyoja (Featherweight).
Shauri anayefanya mazoezi yake Ubungo,
Dar es Salaam, maeneo ya Mabibo na anafundishwa na kocha Mzazi anayetamba kuwa na mabondia
wenye nidhamu na vipaji vya hali ya juu.
Ramadhani Shauri ni bondia chipukizi
mwenye umri wa miaka 19 na historia yake ya ngumi inafurahisha kila anayeisoma
na kuisikia. Ana haiba nzuri inayovutia na anafananishwa na bondia Sugar Ray Leonard wa Marekani kutokana
na haiba yake na upiganaji wake.
Sugar
Ray Leonard
alitamba katika miaka ya 70 na 80. Shauri ni Mfalme anayekuja na hivi sasa
anatishia maisha ya mabondia wengi katika bara la Afrika.
Ramadhani Shauri ana nidhamu ya hali ya
juu na maisha yake katika ngumi yanafurahisha kwa jinsi anavyoishi kwa nidhamu
na kufanya mazoezi ya kujijenga katika ngumi. Katika maisha yake anajiepusha
sana na matatizo ambayo vijana wengi wametumbukia kama vile uvutaji wa bangi,
ngono zembe na mambo mengine yasiyo na malengo katika maisha.
Huyu ndiye kweli Mfalme anayekuja katika
ngumi za kulipwa na nchi yetu imepata bahati kubwa sana kuwa na kipaji cha
bondia kama huyu.
Mpambano wa Shauri umepewa jina la “The Rumble in the City of Heaven’s Peace”
(Vurumai katika Jiji la Amani).
Friday, July 20, 2012
Monday, June 18, 2012
Ukoo mkubwa kuliko maelezo
Mapema kwaka 2000 nilipewa jukumu la kumtambulisha mgeni kwa kundi la wenyeji waliofika kumpokea huyo mgeni nyumbani Butiama. Kabla ya mgeni kufika nilichukuwa kalamu na karatasi na kumuuliza aliye karibu nami jina lake na akanitajia jina na ubini wake. Cha ajabu, alikuwa na ubini kama wangu. Baadaye niligundua kuwa ni mmoja wa baba zangu wadogo.
Niliona aibu sana, lakini naamini kuwa ninayo sababu nzuri ya kutomfahamu. Marehemu babu yangu, Mtemi Nyerere Burito, alikuwa na wake 22. Aidha alikuwa na kina mama wa nyumba ndogo wanne ambao kwa kabila la Wazanaki wanajulikana kama vitungo. Kutokana na uzao wa babu na wake zake, mimi nina ndugu na jamaa wanaokaribia 6,000 kwa hiyo kumfahamu kila mmoja wao siyo jambo rahisi.
Kwa kawaida, uzao uliyonitangulia ulikuwa na watoto wengi, lakini iwapo nitachukuwa wastani wa watoto sita tu kwa kila mme na mke kwa ajili ya kukadiria idadi ya uzao wa Mtemi Nyerere, nikianza na bibi zangu ishirini na wawili, napata idadi ya baba wadogo/shangazi 132, watoto wa baba wadogo/shangazi 792, na wajukuu wa baba wadogo/shangazi 4,752, ikiwa ni jumla ya ndugu 5,676. Na hii ni kutoka upande wa baba mzazi tu.
Hivi karibuni nilikutana na binamu zangu wawili ambao mama yao, marehemu shangazi yangu, ni binti wa tatu wa mke wa saba wa Mtemi Nyerere Burito. Pamoja na kuwa anakaribia miaka 50, mmoja wa wale binamu zangu hakuwa ananifahamu, na alikuwa hajawahi kusikia jina langu. Ilikuwa ni faraja kubwa sana kwangu kwa sababu ilikuwa ni ushahidi tosha kwangu kuwa tatizo la kutoweza kuwatambua ndugu zaidi ya 5,000 halikuwa linawakumba tu wale waliokaa sana jijini Dar es Salaam.
Niliona aibu sana, lakini naamini kuwa ninayo sababu nzuri ya kutomfahamu. Marehemu babu yangu, Mtemi Nyerere Burito, alikuwa na wake 22. Aidha alikuwa na kina mama wa nyumba ndogo wanne ambao kwa kabila la Wazanaki wanajulikana kama vitungo. Kutokana na uzao wa babu na wake zake, mimi nina ndugu na jamaa wanaokaribia 6,000 kwa hiyo kumfahamu kila mmoja wao siyo jambo rahisi.
![]() |
| Sehemu ya wanaukoo wa Burito Nyerere wakiwa |
Friday, June 15, 2012
Mwanzo wa msafara wa Mlima Kilimanjaro
Tarehe 10 Juni 2012 nimemaliza msafara mwingine wa kukwea Mlima Kilimanjaro nikiwa pamoja na kundi la watu 14 katika msafara uliyokuwa na madhumuni ya kuchangisha pesa kwa ajili ya ujenzi wa maktaba ya Shule ya Sekondari Nyegina.
Kutegemea na njia inayotumika, msafara wa kwenda kilele cha Mlima Kilimanjaro unachukuwa kati ya siku 5 hadi 10. Msafara wetu ulichukuwa siku 7 kwenye njia ya Lemosho inayoanzia kwenye lango la Londrossi.
Katika siku ya pili ya msafara, kilele cha Kibo kilionekana mbele yetu kwenye uwanda wa juu wa Shira na kumpa kila mmoja shauku ya kufika kileleni. Wawili kati ya ya 14 tulioanza hawakufanikiwa kufika kileleni. Habari kamili zitawekwa hapa hivi karibuni.
Kutegemea na njia inayotumika, msafara wa kwenda kilele cha Mlima Kilimanjaro unachukuwa kati ya siku 5 hadi 10. Msafara wetu ulichukuwa siku 7 kwenye njia ya Lemosho inayoanzia kwenye lango la Londrossi.
Katika siku ya pili ya msafara, kilele cha Kibo kilionekana mbele yetu kwenye uwanda wa juu wa Shira na kumpa kila mmoja shauku ya kufika kileleni. Wawili kati ya ya 14 tulioanza hawakufanikiwa kufika kileleni. Habari kamili zitawekwa hapa hivi karibuni.
Waziri Bernard Membe naye atabiri hali ngumu kwa Chama cha Mapinduzi
Nimewahi kuandika hapa kuwa majaliwa ya Chama cha Mapinduzi kuelekea kwenye uchaguzi mkuu wa 2015 hayaonekani kuwa mazuri kutokana na mambo kadhaa, ikiwa ni pamoja na:
1. kuongezeka kwa nguvu ya kisiasa ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)
2. kuendelea kupoteza majimbo ya uchaguzi, ikiwa ni pamoja na jimbo la Arumeru hivi karibuni
3. kuachana na misingi iliyokitambulisha Chama cha Mapinduzi kama mwakilishi wa maslahi ya Watanzania wanyonge, wakulima na wafanyakazi.
Habari kamili ziko hapa:
http://muhunda.blogspot.com/2012/04/chama-cha-mapinduzi-ukingoni.html
Sasa, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, naye anatabiri hali mbaya kwa CCM. Habari zake kamili hizi hapa:
http://swahilivilla.blogspot.com/2012/06/aitabiria-ushindi-chadema-uchaguzi-mkuu.html?spref=fb
Ukiona kiongozi mwandamizi wa chama tawala naye anatoa hoja kama hizi ni vugumu kuendelea kusema kuwa ni hoja za watu wasiokitakia mema Chama cha Mapinduzi. Hazibaki kuwa ni ndoto za wapinzani sasa.
1. kuongezeka kwa nguvu ya kisiasa ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)
2. kuendelea kupoteza majimbo ya uchaguzi, ikiwa ni pamoja na jimbo la Arumeru hivi karibuni
3. kuachana na misingi iliyokitambulisha Chama cha Mapinduzi kama mwakilishi wa maslahi ya Watanzania wanyonge, wakulima na wafanyakazi.
Habari kamili ziko hapa:
http://muhunda.blogspot.com/2012/04/chama-cha-mapinduzi-ukingoni.html
Sasa, Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Bernard Membe, naye anatabiri hali mbaya kwa CCM. Habari zake kamili hizi hapa:
http://swahilivilla.blogspot.com/2012/06/aitabiria-ushindi-chadema-uchaguzi-mkuu.html?spref=fb
Ukiona kiongozi mwandamizi wa chama tawala naye anatoa hoja kama hizi ni vugumu kuendelea kusema kuwa ni hoja za watu wasiokitakia mema Chama cha Mapinduzi. Hazibaki kuwa ni ndoto za wapinzani sasa.
Thursday, June 14, 2012
Francis Cheka kupambana na Joseph Kaseba siku ya Saba Saba
Bingwa wa IBF wa Afrika wa uzito wa Super Middleweight, Francis Cheka, ataingia ulingoni tarehe 7 Julai 2012 kupambana na Joseph Kaseba katika pambano linaloandaliwa na Global na kuratibiwa na Kaike
Siraju.
Cheka alitwaa ubingwa wa mabara wa IBF afrika alipomshinda Mada Maugo katika pambano liliofanyika ukumbi wa PTA Dar es Salaam tarehe 28 Aprili 2012.
Pambano hilo litakuwa pambano la kwanza kufanyika katika uwanja mpya wa Taifa wa Dar es Salaam. Baadhi ya mapambano yatakayosindikiza pambano hilo ni pamoja na Adiphoce Mchumia dhidi ya Ramadhani Kido, Amos Mwamakula dhidi ya Rashini Ali, Mkongo Kanda Kabongo dhidi ya Said Mbelwa, na bondia chipukizi Ibrahimu Class toka kambi ya masumbwi Ilala inayonolewa na kocha Habibi Kinyogoli atapambana na Sadiki Momba.
Picha na habari kwa hisani ya superdboxingcoach.
![]() |
| Francis Cheka, kushoto, na Joseph Kaseba, kulia. |
Cheka alitwaa ubingwa wa mabara wa IBF afrika alipomshinda Mada Maugo katika pambano liliofanyika ukumbi wa PTA Dar es Salaam tarehe 28 Aprili 2012.
Pambano hilo litakuwa pambano la kwanza kufanyika katika uwanja mpya wa Taifa wa Dar es Salaam. Baadhi ya mapambano yatakayosindikiza pambano hilo ni pamoja na Adiphoce Mchumia dhidi ya Ramadhani Kido, Amos Mwamakula dhidi ya Rashini Ali, Mkongo Kanda Kabongo dhidi ya Said Mbelwa, na bondia chipukizi Ibrahimu Class toka kambi ya masumbwi Ilala inayonolewa na kocha Habibi Kinyogoli atapambana na Sadiki Momba.
Picha na habari kwa hisani ya superdboxingcoach.
Subscribe to:
Posts (Atom)
.jpg)


