Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Tuesday, April 3, 2012

Chama cha Mapinduzi ukingoni?

Katika miaka ya hivi kariubuni Chama cha Mapinduzi (CCM) kimejikuta kikaangoni mara kwa mara kutokana na mpambano mkali wa kisiasa ambao unaletwa kwake na vyama vya upinzani, hasa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA). Sasa dalili zinaonyesha CCM inaelekea ukingoni.

Kwenye kura zilizopigwa tarehe 1 Aprili 2012, CCM kimeshindwa kwenye uchaguzi mdogo wa jimbo la Arumeru lililoachwa wazi kutokana na kifo cha mbunge wake, Jeremiah Sumari, ambaye alikuwa mwanachama wa CCM.

Kwamba wapiga kura walewale waliyomchagua mwanachama wa CCM kuwa mbunge wao mwaka 2010 wameamua sasa kuchagua mgombea wa CHADEMA ni ishara dhahiri kuwa CCM inaendelea kupoteza imani ya Watanzania wengi.

Ni mwanzo wa mwisho wa CCM kama chama tawala? Tuanze mazoezi ya kumwita mwanachama wa chama cha upinzani “Mheshimiwa Rais”? Jibu litategemea iwapo CCM kitajiangalia upya na kuirejesha misingi ambayo ilikifanya kuwa chama kilichopigania maslahi ya wakulima na wafanyakazi. Baada ya hilo, itategemea kwa kiasi kikubwa nani atateuliwa na CCM kuwa mgombea wa urais kwenye uchaguzi mkuu ujao wa 2015.

CCM wakiendelea na muenendo wao wa sasa, muda si mrefu watahamia kwenye benchi za upinzani bungeni.

No comments: