Majuma kadhaa yaliyopita nilihojiwa na mwandishi wa habari wa Mwanza kuhusu maoni yangu juu ya wagombea urais waliojitokeza kuwania nafasi ya urais kwenye uchaguzi mkuu mwaka huu.
Sehemu ya mahojiano hayo imechapishwa hapa.
Saturday, March 14, 2015
Saturday, January 24, 2015
Waheshimiwa wengi sana Tanzania
Neno mheshimiwa limekosa heshima inayokusudiwa kwa maoni yangu.Sababu kubwa ni kuwa Tanzania ina waheshimiwa wengi sana.
Sizungumzii wale watu ambao nafasi zao katika jamii zinatulazimu kuwaita "waheshimiwa", kwa mfano mahakimu, majaji, na wabunge. Nazungumzia tabia iliyojengeka ya matumizi ya "mheshimiwa" kwa kila raia anayezungumza Kiswahili.
Mimi nilidhani kuwa madhumuni ya kutumia "mheshimiwa" haina tofauti sana na kumuita mtu daktari. Madhumuni ni kumpambanua kama mtu mwenye nafasi muhimu katika jamii ambayo inahitaji kuweka mipaka ya namna watu wengine wanavyowasiliana nae, au kubainisha kuwa ni mtu ambaye anayo taaluma maalum. Kwa upande wa majaji na mahakimu ni viongozi ambao wana majukumu muhimu ndani ya jamii na wanapata upendeleo fulani kwa namna wanavyochukuliwa na jamii. Kwa kuwapa huo upendeleo jamii pia inategemea kuwa waheshimiwa watakuwa watu wanaojiheshimu mbele ya jamii.
Sasa cheo hiki anapopewa kila mtu kuna hatari ya kukigawa kwa watu ambao hawajiheshimu hata chembe na ambao wataharibu maana halisi ya uheshimiwa. Kwa maoni yangu waheshimiwa wanaosimamia kesi mahakamani ndiyo wanastahili zaidi kuitwa waheshimiwa.
Sisi tuliobaki tungerudia kuitana ndugu, ingawa wengi wanaamini undugu unahusiana na siasa ya Ujamaa peke yake. Siyo kweli. Tumsikilize Rais Mstaafu Mkapa, akizungmuza kwenye semina ya Muafaka ya Vyama vya Siasa, Zanzibar, tarehe 7 Machi 2005:
"Ndugu siyo neno la kiitikadi tu, linahusu pia utamaduni wetu. Mtaniwia radhi nikiwaita "Ndugu wanasemina."
Wewe ni ndugu au mheshimiwa?
Sunday, January 11, 2015
Kandambili, rangi mbili
Sehemu nyingi za Tanzania, hasa kwenye miji midogo, ukiingia kwenye gesti au hoteli basi kama umewekewa kandambili chumbani utakuta kila moja ina rangi tofauti.
Sababu kubwa ni kuwa baadhi ya wateja wanaoingia kwenye sehemu hizi siyo waaminifu na wanapoondoka huamua kuondoka na kandambili. Inaaminiwa kuwa zikiwa zina rangi mbili tofauti basi mwenye kusudio la kuziiba ataacha kufanya hivyo. Sina hakika kama inasaidia kuzuwia wizi.
Saturday, December 13, 2014
Mwisho wa kampeni Butiama za uchaguzi wa serikali za mitaa
Viongozi na wagombea wa Chama cha Mapinduzi wa kijijini Butiama wakiomba kura mbele ya wakazi wa Butiama siku moja kabla ya uchaguzi wa serikali za mitaa utakaofanyika nchini kote kesho tarehe 14 Desemba 2014.
Mkutano huu (picha ya juu) ulifanyika eneo la stendi, Butiama. Wapinzani wao wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) walifanya mkutano wa mwisho wa kampeni kwenye kitongoji cha Mtuzu, Butiama.
Friday, December 12, 2014
Mabondia na unga (sehemu ya tatu ya awamu tatu)
Promota wa ndondi za kulipwa, Ibrahim Kamwe, anaeleza kwa nini baadhi ya mabondia wanajiingiza kwenye biashara ya madawa ya kulevya.
![]() |
| Ibrahim Kamwe |
Ukiangalia umbumbumbu na maskini tulionao mabondia, hapo wajanja
wenye pesa zao, wafanyabiashara, na baadhi ya viongozi wanatumia udhaifu
tulionao mabondia kutuhadaa kwa kutupatia safari za nje za kimichezo au
matembezi ya kwenda kufanya mazoezi ughaibuni na hatimaye kutubebesha
mihadarati (madawa ya kulevya) bila kujua kwa kutuwekea katika mizigo tunayosafiri
nayo. Wakati mwingine kuna baadhi ya wafanya biashara hao wenye pesa zao
hukuweka wazi wakati unaenda pigana umbebee mzigo wake na atakulipa pesa
nyingi. Hapo ndipo tunapobanwa ukiangalia nyumbani tunalalia telemka tukaze,
tunashindia tembele mlo mmoja, msosi wa kengele tena kwa masimango,
mfukoni huna kitu na wala huna kazi itakayokupatia pesa ya kula kwa wakati huo. Hapo sijaingiza mambo ya kodi, na demu wangu namlinda vipi.
Hii njaa na umaskini tulio nao mabondia ndiyo inawapa nguvu vigogo
kututumia kwa kutubebesha madawa ya kulevya kusafirisha nje wakijua wazi
hatuwezi kataa kutokana na dhiki tuliyo nayo. Tutakubali tu kwani hakuna
apendae kulala njaa, kulala pachafu, au kuvaa midabwada.
“Siwezi acha dili la pesa kama hili wakati jina langu kubwa kila kona linatajwa mitaani na vyombo vya habari lakini mimi binafsi nauli ya daladala sina. Siku ya tatu leo nakula mlo mmoja kwa siku, watoto hawapo katika hali nzuri, mazoezi yenyewe sifanyi kwa raha nafikiria nitapata wapi mshiko. Leo unaniletea ishu ya pesa niikatae si nitakuwa kichaa?”
“Wadau wenzangu wa ngumi ,wapambe wao, na walio karibu na sisi mabondia wana nguo za bei kubwa wanapendeza, wana magari. Ukiangalia mimi bondia ndiye mtendaji wao mkuu nipo ovyo sina kitu mfukoni wala tumboni, madeni kibao yaani majanga matupu.”
Ushauri wangu kwa serikali au taasisi zinazohusika na
wanaolichukia jambo hili kiukweli - maana wengine hujifanya kulichukia mdomoni
pembeni ndiyo watendaji wakuu wa kuwatumia wanamichezo au wasanii kwa faida zao
- mabondia au wanamichezo tuboreshewe maeneo yetu ya michezo ikiwemo katika
vilabu vyetu na maeneo ya mazoezi, na vifaa viongezwe. Ikiwezekana kodi ya
vifaa vya michezo ipunguzwe ili viwe vingi nchini mabondia wasibabaike na vya
kuazima au kuangalia katika TV vifaa vya wenzetu.
Serikali iwajali mabondia, isaidie kudhamini semina za walimu wa
ngumi ili wawaongoze vyema vijana wao. Magym ya makusudi yajengwe na maeneo ya
wazi wasigawane wenye pesa na viongozi kwa faida zao. Wajenge sehemu za michezo
ya ndani, na kama pia
itatumika njia ya kutoa madarasa matupu katika mashule yetu kwa ajili ya
kutuachia sehemu ya mazoezi ya jioni itasaidia sana kukuza mchezo na walimu
wenye taaluma kufundisha vizuri kuliko mabondia kufundishana vichochoroni na
kutokuwa na nidhamu ya mchezo wala maisha.
Subscribe to:
Posts (Atom)
.jpg)
.jpg)
%2B(640x480).jpg)
