Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Saturday, November 11, 2017

Mimba zisizoisha za Chausiku Suleiman

Zaidi ya miaka sita iliyopita nilipata fursa ya kumtembelea mama mmoja, Chausiku Suleiman, anayeishi Maji Chai, jirani na Tengeru kwenye barabara kuu ya kutoka Moshi kwenda Arusha. Alinipa simulizi za ajabu. Yeye anapata ujauzito kila anapojifungua, bila hata kukutana na mume wake.

Nilipoonana naye alikuwa na umri wa miaka 47 na alikuwa na watoto 16 aliyewazaa ndani ya kipindi cha miaka 30. Tatizo lake lilianza alipopata ujauzito wa mtoto wa tano. Majuma matatu baada kujifungua alihisi kuwa alikuwa mjamzito tena. Nilipoonana naye mwaka 2011 alisema kuwa mimba yake wakati huo ilikuwa ina zaidi ya miaka mitatu.

Chausiku Suleiman akiwa na baadhi ya watoto wake, Maji Chai, Arusha.
Nilipomuuliza iwapo ametafuta ushauri wa daktari aliniambia kuwa madaktari wameshindwa kubaini tatizo lake na wameshindwa kuona kama ana kichanga tumboni.

Alisema anahisi kuwa madaktari wanaamini kuwa ana imani kuwa na tatizo ambalo halipo.

No comments: