Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Tuesday, December 13, 2016

Lugha yetu Kiswahili

Kiswahili lugha nzuri, lakini hutatanisha wengi.

Siku moja nikiwa safarini nilijikuta kwenye mgahawa wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro. Nilikuwa nimewahi asubuhi mapema siku hiyo nikaondoka Arusha bila kupata staftahi, au kifungua kinywa.

Nilipovuka eneo la ukaguzi la maafisa usalama na kuingia kwenye ukumbi wa abiria wanaojiandaa kupanda ndege nikawahi kwenye mgahawa na kuagiza kahawa. Aidha, hupendelea kula mayai asubuhi, kwa hiyo nikamuita mhudumu ili nimuagize mayai kuwahi kabla ya abiria kutangaziwa kuingia ndani ya ndege.

Mazungumzo yakawa hivi:

Mimi: Nitapata mayai?
Yeye: Ndiyo.
Mimi: Naomba jicho la ng'ombe.
Yeye: Hapa hatuna jicho la ng'ombe.

Sikumuelewa. Huyo huyo aliyekubali kuwa mayai yapo akaniambia hawana jicho la ng'ombe. Nilibaini naongea na mtu ambaye Kiswahili kinampiga chenga. Nilihisi alikuwa mwenyeji wa Kenya. Nikamwambia anipeleke kwa mpishi niongee naye, na huko kwa mpishi nikaagiza mayai jicho la ng'ombe na yakakaangwa vizuri tu.
Jicho la ng'ombe.
Nilivyoelewa mimi, mhudumu alidhani nimeagiza nipikiwe jicho hasa la ng'ombe.

Taarifa inayofanana na hii:
http://muhunda.blogspot.com/2013/10/msiofahamu-vyema-kiingereza-zungumzeni.html

No comments: