Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Wednesday, March 9, 2011

Msanii Hardman ateuliwa katika Tuzo za Muziki za Kilimanjaro

Kwa mujibu wa taarifa iliyopokelewa toka kampuni ya Maisha Music, msanii wake, Hardman, ameteuliwa kushindania Tuzo ya Muziki ya Kilimanjaro Kilimanjaro,
Bango la Hardman la uzinduzi wa album yake, Imebaki Stori, uliyofanyika Desemba 2010
Taarifa hiyo pia inatoa wito na maelekezo kwa mashabiki wa Hardman kumpigia kura ili aweze kushinda.
Taarifa kamili hii hapa: 
Toleo hili la barua taarifa limejikita zaidi juu ya uteuzi wa Hardmad ni msanii wa reggae na dancehall ambaye kwa sasa anasimamiwa na kampuni ya Maisha Music. Katika tuzo za mwaka huu amefanikiwa kuteuliwa katika vipengele viwili navyo ni; kipengele cha wimbo bora wa reggae ambapo ameingiza ameingiza nyimbo mbili, na kipengele kingine ni kile cha wimbo bora wa kushirikishwa, na ni kutokana na kushirikishwa kwake katika wimbo wa Mwana FA na AY “Dakika Moja”.  

Haya ni mafanikio makubwa kwetu pamoja na Hardmad, na tunaamini kuwa hii imetokana na kujituma kwake kwa bidii pamoja na ushirikiano baina yetu. Sisi tunamtakia kila la heri katika tukio hili muhimu kwa maisha yake kama msanii. Maisha Music inapenda pia kuwatakia mafanikio marafiki zetu wengine ambao wamo katika kinyangányiro hiki mwaka huu, baadhi yao ni Jhikoman, Warriors From The East, Ras Rwanda, Lamar, Fid Q, Ray C na Chidi Beenz.

Washindi wa tuzo za Kilimanjaro wanapatikana kwa kupiga kura. Hii inamaanisha kwamba wimbo utakaopata kura nyingi kutoka kwa mashabiki na wapenzi ndiyo utakoshinda. Tafadhali mpigieni Hardmad kura zenu kwa wingi ili aweze kufanikiwa kuibuka kidedea kwani tunaamini anastahili na unaweza kuthibitisha kwa kusikiliza kazi zake kupitia katika linki zilizowekwa hapo chini.

Unaweza kumpigia kura kwa njia mbili tofauti ambazo ni; kwa kubonyeza katika linki iliyoonyeshwa hapo chini na pili ni kwa kutuma ujumbe mfupi wa simu. Iwapo utaweza basi unayo ruhusa ya kutumia njia zote mbili. Angalizo: Kwa kuwa Hardmad ana nyimbo mbili katika kipengele kimoja tunapendda kuwashauri wadau wetu kuupigia kura wimbo wa Ujio Mpya ambao amemshirikisha Enika. Vinginevyo kunaweza kuwa na uwezekano wa kura kugawanyika katika nyimbo mbili.

Katika wimbo wa Ujio mpya tumeshangaa kuona kuwa limeongezwa jina geni la msanii ambaye hatumfahamu (BNV). Tunadhani kuna makosa
yamefanyika na tunajaribu kuwasiliana na wahusika ili kuona namna ya kuliondoa.

Namna ya kupiga kura:

KWA MTANDAO (rahisi sana): 

Gonga kwenye linki hii: http://www.kilitime.co.tz/awards/2009/nominees_2007.php (Na ni kwa mwaka 2011), na ikifunguka gonga kwenye nyimbo unazotaka kuzipigia kura, andika anuani yako ya barua pepe na bonyeza “VOTE”. Kumbuka kubonyeza katika linki ya kuhakiki na utatumiwa barua pepe ya kutoka KTMA (Kilimanjaro Tanzanian Music Awards), vinginevyo kura yako haitasajiliwa! Unaweza kupiga kura moja tu kwa anuani moja ya barua

SIMU:

"Wimbo bora wa Reggae":

Andika K179 katika ujumbe mfupi na tuma kwa namba 15747 ili kuupigia kura wimbo wa "Ujio Mpya - Hardmad Feat. Enika" 
Andika K186 katika ujumbe mfupi na tuma kwa namba 15747 ili kuupigia kura wimbo wa "What you feel inside - Hardmad"

(Unaweza kupiga kura moja tu katika kila kipengele kwa kila namba ya simu).

"Wimbo bora wa kushirikishwa:

Andika W137 kwa ujumbe mfupi na kisha tuma kwa namba 15747 ili kuupigia kura wimbo wa "Dakika Moja - Mwana FA & AY feat. Hardmad" 

Tunakushukuru sana kwa ushirikiano wako na msaada ambao tunaamini utaweza kumfikisha Hardmad katika kilele cha mafanikio anayostahili. Tuna matarajio ya mengi mazuri katika harakati za kimuziki kwetu pamoja na wasanii tunaoshirikiana nao. Kwa ufafanuzi zaidi unaweza kusikiliza na kuangalia baadhi ya nyimbo katika Myspace au Youtube au kwenye kurasa za Hardmad katika mitandao ya Facebook na Myspace. Albamu mpya ya Hardmad “Imebaki Story” kwa sasa inapatikana pia kwa njia ya mtandao, na unaweza kuipata kwa kubonyeza hapa kwa Itunes pamoja na maduka mengine ya kwenye mtandaoni. 

Hivi sasa Maisha Music ipo katika maandalizi ya maonyesho kadhaa ya utambulisho wa albamu ya Hardmad katika miji mbalimbali hapa Tanzania pamoja na Kenya mwezi wa Aprili. Taarifa sahihi pamoja na tarehe zitatangazwa muda si mrefu.

Tafadhali tusaidie kusambaza taarifa hii kwa wapendwa, marafiki pamoja na wadau wengiine wa muziki!

Kila la heri na asante sana kutoka
Timu ya MAISHA MUSIC