Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Thursday, October 27, 2011

Waziri Mary Nagu azindua ofisi ya kituo cha uekezaji Mbeya


Taarifa zifuatazo zimetolewa na blogu ya Mbeya Yetu:

Waziri Mary Nagu amezindu ofisi ya kanda ya Kituo cha Uwekezaji mjini Mbeya juma liliopita.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwezeshaji na Uwekezaji), Dk. Mary Nagu akikata utepe kuzindua ofisi ya kituo cha uwekezaji (TCI) nyanda za juu kusini mjini Mbeya.
Akizindua ofisi hiyo mwishoni mwa wiki jijini Mbeya, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwezeshaji na Uwekezaji), Dk. Mary Nagu alisema ofisi hiyo ni muhimu katika kusaidia wajasiriamali na wawekezaji wa mikoa ya Ruvuma, Iringa Rukwa na Mbeya kuitumia kwa ajili ya kuanzisha miradi mbalimbali ya uwekezaji.

Ufunguzi huo pia ulihudhuriwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Kituo cha Uwekezaji, Balozi Elly Mtango, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Raymond  Mbilinyi, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro.

Monday, October 10, 2011

Mbwana Matumla ajiandaa kwa pambano dhidi ya Francis Miyeyusho

Mabondia Mbwana Matumla (kushoto) na Mussa Sunga (kulia) wakipigana wakati wa mazoezi ya kambi ya Ilala Dar es salaam hivi karibuni. Kulia ni kocha Mohamedi Chipota. 
Matumla anajiandaa na mpambano wake wa ubingwa dhidi ya Francis Miyeyusho litakalofanyika mwishoni mwa mwezi huu.(Picha na habari kwa hisani ya www.superdboxingcoach.blogspot.com)

Siku ya Nyerere, 14 Oktoba, kuadhimishwa Washington D.C.


Taarifa hii imetolewa na Mubelwa T. Bandio:
Maadhimisho ya nne ya kuenzi maisha na kazi za Mwl Julius K. Nyerere yatafanyika Oktoba 15, 2011 hapa Washington DC
Mmoja wa waasisi wa Julius Nyerere Commemoration Bwn Rick Tingling anaelezea maandalizi ya siku hiyo katika video hapa chini:

NYOTE MNAKARIBISHWA

Itafanyika 
Howard University Basement Auditorium
725, 2225 Georgia Ave, NW, Washington, DC 20059
FROM 3PM-6PM

MAELEKEZO KUELEKEA Howard University Hospital Basement Auditorium:

  1. Ingilia mlango wa mbele wa Hospitali unaotazamana na Georgia Avenue.
  2. Pita kwenye dawati la maelezo kwa utambulisho
  3. Endelea mbele mpaka kwenye "lift" zilizo kama yadi 50 toka dawati la mapokezi.
  4. Chukua "lift" / elevator kuelekea sakafu ya chini (basement).
  5. Elekea upande wa kulia ukifuata alama zinazoelekeza ulipo ukumbi.
AMBATANISHO: MAELEZO KUHUSU MAADHIMISHO HAYO.
NOTE: Mabadiliko pekee niliyojulishwa ni kuwa Balozi Mwanaidi Maajar hataweza kuhudhuria kwa kuwa atakuwa nje ya mji.