Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Friday, July 20, 2012

Mtanzania Ramadhani Shauri kupambana na Mganda Sande Kizito kuwania ubingwa wa mabara wa IBF Afrika

Mtanzania Ramadhani Shauri atapanda ulingoni siku ya Idd pili kupambana na bondia Sande Kizito kutoka Uganda kugombea mkanda wa IBF katika bara la Africa katika uzito wa unyoja (Featherweight).

Shauri anayefanya mazoezi yake Ubungo, Dar es Salaam, maeneo ya Mabibo na anafundishwa na kocha Mzazi anayetamba kuwa na mabondia wenye nidhamu na vipaji vya hali ya juu.

Ramadhani Shauri ni bondia chipukizi mwenye umri wa miaka 19 na historia yake ya ngumi inafurahisha kila anayeisoma na kuisikia. Ana haiba nzuri inayovutia na anafananishwa na bondia Sugar Ray Leonard wa Marekani kutokana na haiba yake na upiganaji wake.
Ramadhani Shauri, katikati, akiwa ameshika mkanda atakaoupigania dhidi ya bondia Sande Kizito. Kulia ni promota wa pambano, Lucas Rutainurwa na kushoto ni mwandishi wa blogu hii na ambaye pia ni Makamu wa Rais wa Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBC), Madaraka Nyerere.
Sugar Ray Leonard alitamba katika miaka ya 70 na 80. Shauri ni Mfalme anayekuja na hivi sasa anatishia maisha ya mabondia wengi katika bara la Afrika.

Ramadhani Shauri ana nidhamu ya hali ya juu na maisha yake katika ngumi yanafurahisha kwa jinsi anavyoishi kwa nidhamu na kufanya mazoezi ya kujijenga katika ngumi. Katika maisha yake anajiepusha sana na matatizo ambayo vijana wengi wametumbukia kama vile uvutaji wa bangi, ngono zembe na mambo mengine yasiyo na malengo katika maisha.

Huyu ndiye kweli Mfalme anayekuja katika ngumi za kulipwa na nchi yetu imepata bahati kubwa sana kuwa na kipaji cha bondia kama huyu.

Mpambano wa Shauri umepewa jina la “The Rumble in the City of Heaven’s Peace” (Vurumai katika Jiji la Amani).