Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Saturday, January 24, 2015

Waheshimiwa wengi sana Tanzania

Neno mheshimiwa limekosa heshima inayokusudiwa kwa maoni yangu.Sababu kubwa ni kuwa Tanzania ina waheshimiwa wengi sana.

Sizungumzii wale watu ambao nafasi zao katika jamii zinatulazimu kuwaita "waheshimiwa", kwa mfano mahakimu, majaji, na wabunge. Nazungumzia tabia iliyojengeka ya matumizi ya "mheshimiwa" kwa kila raia anayezungumza Kiswahili. 

Mimi nilidhani kuwa madhumuni ya kutumia "mheshimiwa" haina tofauti sana na kumuita mtu daktari. Madhumuni ni kumpambanua kama mtu mwenye nafasi muhimu katika jamii ambayo inahitaji kuweka mipaka ya namna watu wengine wanavyowasiliana nae, au kubainisha kuwa ni mtu ambaye anayo taaluma maalum. Kwa upande wa majaji na mahakimu ni viongozi ambao wana majukumu muhimu ndani ya jamii na wanapata upendeleo fulani kwa namna wanavyochukuliwa na jamii. Kwa kuwapa huo upendeleo jamii pia inategemea kuwa waheshimiwa watakuwa watu wanaojiheshimu mbele ya jamii.

Sasa cheo hiki anapopewa kila mtu kuna hatari ya kukigawa kwa watu ambao hawajiheshimu hata chembe na ambao wataharibu maana halisi ya uheshimiwa. Kwa maoni yangu waheshimiwa wanaosimamia kesi mahakamani ndiyo wanastahili zaidi kuitwa waheshimiwa.

Sisi tuliobaki tungerudia kuitana ndugu, ingawa wengi wanaamini undugu unahusiana na siasa ya Ujamaa peke yake. Siyo kweli. Tumsikilize Rais Mstaafu Mkapa, akizungmuza kwenye semina ya Muafaka ya Vyama vya Siasa, Zanzibar, tarehe 7 Machi 2005:

"Ndugu siyo neno la kiitikadi tu, linahusu pia utamaduni wetu. Mtaniwia radhi nikiwaita "Ndugu wanasemina."

Wewe ni ndugu au mheshimiwa?

Sunday, January 11, 2015

Kandambili, rangi mbili

Sehemu nyingi za Tanzania, hasa kwenye miji midogo, ukiingia kwenye gesti au hoteli basi kama umewekewa kandambili chumbani utakuta kila moja ina rangi tofauti.
Sababu kubwa ni kuwa baadhi ya wateja wanaoingia kwenye sehemu hizi siyo waaminifu na wanapoondoka huamua kuondoka na kandambili. Inaaminiwa kuwa zikiwa zina rangi mbili tofauti basi mwenye kusudio la kuziiba ataacha kufanya hivyo. Sina hakika kama inasaidia kuzuwia wizi.