Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Sunday, November 20, 2016

Rais Magufuli na ngoma za Ikulu: utamaduni unadumishwa

Desturi ya kupokea mgeni mashuhuri kwa kupiga ngoma ipo miongoni mwa watawala wa makabila mengi ya Tanzania.

Enzi za tawala za kitemi, hiyo ndiyo ilikuwa desturi. Mgeni, hasa yule ambaye alikuwa na hadhi ya utawala kama mwenyeji wake, alipigiwa ngoma za mwenyeji wake. Ni ngoma ambazo zilisikika kwenye himaya ya mtemi mwenyeji na zilisambaza taarifa ya kuwepo kwa mgeni muhimu.

Baada ya uhuru wa Tanganyika, desturi hiyo ilihamia kwenye Ikulu ya Dar es Salaam na viongozi mbalimbali waliotembelea Ikulu walipokelewa kwa desturi hiyo.
Rais Nyerere akimkaribisha Rais Sekou Toure wa Guinea kupiga ngoma za kumkaribisha Ikulu, Dar es Salaam.
Kumbukumbu yangu inaweza kuwa siyo sahihi, lakini sikumbuki kama baada ya Mwalimu Nyerere desturi hii ilifuatwa sana, ingawa tunaona sasa kuwa Rais wa awamu hii ya tano, John Magufuli, ameichangamkia vyema na huwashirikisha viongozi wanaofika Ikulu kupiga ngoma zilizopo Ikulu.

Inawezekana pia kuwa siyo wageni wote wanaofika Ikulu ambao hukaribishwa kwa kupiga ngoma,

Thursday, November 10, 2016

Mbuga ya Serengeti inavyoonekana juu ya Mlima Balili

Mkoa wa Mara una vivutio vingi vya utalii, na mojawapo ya vivutio hivi ni Mlima Balili uliyopo Wilaya ya Bunda.
Kutoka juu ya Mlima Balili kuna mojawapo ya mandhari nzuri katika eneo hili. Kwenye picha, upande wa kushoto ni Hifadhi ya Taifa ya Serengeti. Juu kidogo ya picha hii unaoenakana Mto Grumeti ambao ni mojawapo ya mito inayotiririka ndani ya Hifadhi ya Serengeti na kuishia ndani ya Ziwa Victoria.

Ziwa Victoria linaonekana juu kulia. Upande wa kulia ni barabara kuu inayotoka Musoma hadi Mwanza.