Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Tuesday, April 26, 2011

Mwalimu wangu, Gordian Mukiza

Mwaka jana, wakati vuguvugu za kampeni za Uchaguzi Mkuu zikiendelea nchini kote, nilifunga safari kwenda Muleba, Kagera, kumtembelea rafiki yangu Hamisi Millanga, aliyekuwa kwenye mikakati ya kutetea kiti chake cha udiwani wa kata ya Muleba kupitia Chama cha Wananchi (CUF). Safari yangu ilikuwa na nia ya kupata muelekeo wa harakati za kampeni kwenye maeneo hayo.
Mwalimu Gordian Mukiza, kushoto, na mimi.
Siku moja katika pitapita zangu mjini Muleba nilikutana na mwalimu wangu wa siku nyingi nilivyokuwa mwanafunzi wa Shycom (Shinyanga Commercial Institute) kati ya mwaka 1977 – 1979, Mwalimu Gordian Mukiza. Aliyenitambua ni yeye, pamoja na kuwa nimesheheni mvi kibao kichwani na pengine sifanani hata kidogo na nilivyokuwa Shycom.

Aliniambia kuwa alikuwa mgombea wa udiwani wa kata ya Ikondo, Wilaya ya Muleba Kusini, kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM). Alishinda uchaguzi huo kwa kishindo, na matokeo yalikuwa kama ifuatavyo:

Wapiga kura waliyoandikishwa: 2,553
Waliyopiga kura: 1,685
Kura zilizoharibika: 64

Kura za Wagombea:
CHADEMA - Amri Kalizabona Hamisi : 254
CUF - Felician Rutwaza:                   400
CCM - Gordian Joseph Mukiza:          967