Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Sunday, May 18, 2014

Mwanza, juzi

Juzi nikiwa jijini Mwanza, mtu mmoja nisiyemfamu aliniomba pesa. Nilimjibu kuwa sikuwa na pesa za kumpa. Aliendelea kuniomba. Nilisisitiza sikuwa na pesa.

Akasema: "Du! Sasa mheshimiwa unaniacha na hali mbaya sana."

Mimi: "Vumilia. Leo huna, kesho utapata."

Yeye: "Tutafika kweli? Eti wanasema tusubiri mpaka mwaka 2025 ndiyo mambo yatakuwa mazuri kwetu sisi maskini? Tutakuwa bado tunaishi kweli?

Mimi: "Vumilia. Tutafika."

Niliondoka nikiwaza kuhusu matarajio ya raia mwenzangu kuhusiana  na Visheni ya Maendeleo ya 2025 inayolenga kuifanya Tanzania kuwa nchi ya uchumi wa kati.

Ikifika tarehe 1 Januari 2026 na hali yake iko vile vile patachimbika.

Tuesday, May 13, 2014

Uandishi ni kazi kweli kweli!

Ni muda mrefu sasa sijachapisha habari zozote hapa kwenye blogu yangu. Uandishi wa mara kwa mara siyo kazi ndogo, hasa pale mwandishi anapotarajiwa kuongea jambo la maana kila wakati, na kufanya hivyo mara kwa mara.

Tatizo mojawapo linalonizuwia kuandika mara kwa mara ni kusafiri huku na kule kwa shughuli mbali mbali. Nimejenga mazowea ya kuandika nikiwa sehemu moja tu: nyumbani. Ninaposafiri sipati utulivu wa kutosha kuniwezesha kuandika vyema.

Hata hivyo naweka kando hivyo visingizio na natarajia kuanza tena kuhuisha blogu hii kwa kuweka habari hapa na maoni yangu ya masuala kadha wa kadha.