Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Friday, December 30, 2016

Hii ndiyo redio ya Mwalimu Nyerere 'enzi za Mwalimu'


Hii ndiyo redio ya Mwalimu Nyerere 'enzi za Mwalimu' (kwenye picha, chini). Ni aina ya National Panasonic, ambayo aliitumia katika miaka ya sitini na sabini.

Mwalimu Nyerere alikuwa msikilizaji makini kabisa wa taarifa za habari, na alikuwa akisikiliza taarifa kutoka vituo vya redio vya nje ya nchi, kama Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC), pamoja na vituo vya ndani (wakati huo ikiwa ni Redio Tanzania peke yake).

Uzito wa redio hii ni kilo 20, na wakati wa safari kuna mtu maalum alikuwa akiibeba. Mabadiliko ya teknolojia yalisababisha kupungua kwa ukubwa wa redio, na katika miaka ya baadaye Mwalimu naye alianza kutumia redio ndogo zaidi ambazo uzito ulifikia hata chini ya robo kilo. Redio hii ipo kwenye Makumbusho ya Mwalimu J.K. Nyerere, Butiama.

No comments: