Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Tuesday, March 21, 2017

Tanzania ni nchi nzuri sana

Tanzania ni nchi nzuri sana. Hakuna ubishi juu ya hoja hii.

Lakini inahitaji fursa ya kutoka sehemu moja na kuzunguka maeneo mbalimbali ya Tanzania ambayo yanavutia kwa mandhari na vivutio mbalimbali vya asili. Ukibaki sehemu moja tu huwezi kufahamu juu ya ukweli huu.

Kama huna hiyo fursa siyo kosa lako, lakini kama unayo fursa na uwezo basi huna budi kuzunguka na kuifahamu vyema nchi yako. Utalii wa ndani unajenga uchumi, na wale ambao tunao uwezo wa kutembelea maeneo ya Tanzania tunapaswa kuchangia kwa kadiri tunavyoweza.



Moja ya sehemu ambazo zinavutia nchini Tanzania ni maeneo yanayozunguka Ziwa Viktoria. Video hii imechukuliwa kwenye kivuko cha Busisi kwenye njia kuu inayotumika na wasafiri kati ya Mwanza na Geita, Chato, hadi Kagera.

No comments: