Taarifa iliyotolewa na Sabatho Nyamsenda, Mwenyekiti wa Sauti ya Vijana Tanzania (SAVITA) inaeleza kuwa kongamano la kuadhimisha miaka 44 ya Azimio la Arusha lililokuwa lifanyike leo asubuhi Chuo Kikuu cha Dar es Salaam limeahirishwa.
Sababu ya kuahirishwa imeelezwa kuwa ni "kukosekana kwa hali ya utulivu katika mazingira ya chuo." Taarifa katika vyombo vya habari zinaeleza kuwa jana wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam walipambana na polisi baada ya kujaribu kuandamana kuelekea Ikulu Dar es Salaam kupeleka madai ya kuongezewa posho.
Taarifa ya Nyamsenda haijaeleza ni lini hilo kongamano litafanyika. Taarfia zaidi zinaweza kupatikana kwa Sabatho Nyamsenda 0717 34070/0784 641031.
Saturday, February 5, 2011
Wednesday, February 2, 2011
Kongamano la Azimio la Arusha Jumamosi tarehe 5 Februari 2011
Kongamano la kuadhimisha miaka 44 ya Azimio la Arusha
Siku:
Jumamosi tarehe 5 Februari 2011
Muda:
Saa 3:30 Asubuhi mpaka saa 8:00 Mchana
Mahali:
Ukumbi wa Nkrumah, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam
Kauli Mbiu:
"Tafakuri ya kina juu ya Azimio la Arusha. Je, lina nafasi katika mjadala wa katiba mpya?"
Mtoa mada: Prof. Issa G. Shivji
Waandaaji:
Sauti ya Vijana Tanzania (SAVITA - UDSM) & Philosophy Club
Mawasiliano:
0717 34070/0784 641031 (Sabatho Nyamsenda), na 0713 415001 (Hatib Yusuph)
Subscribe to:
Posts (Atom)