Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Sunday, May 18, 2014

Mwanza, juzi

Juzi nikiwa jijini Mwanza, mtu mmoja nisiyemfamu aliniomba pesa. Nilimjibu kuwa sikuwa na pesa za kumpa. Aliendelea kuniomba. Nilisisitiza sikuwa na pesa.

Akasema: "Du! Sasa mheshimiwa unaniacha na hali mbaya sana."

Mimi: "Vumilia. Leo huna, kesho utapata."

Yeye: "Tutafika kweli? Eti wanasema tusubiri mpaka mwaka 2025 ndiyo mambo yatakuwa mazuri kwetu sisi maskini? Tutakuwa bado tunaishi kweli?

Mimi: "Vumilia. Tutafika."

Niliondoka nikiwaza kuhusu matarajio ya raia mwenzangu kuhusiana  na Visheni ya Maendeleo ya 2025 inayolenga kuifanya Tanzania kuwa nchi ya uchumi wa kati.

Ikifika tarehe 1 Januari 2026 na hali yake iko vile vile patachimbika.

1 comment:

Swahili Trainers and Translators CO LTD said...

Inasikitisha brother kilio cha mnyonge machozi uenda na maji