Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Saturday, July 12, 2014

Wageni wa Butiama: Urmila Jhaveri

Ni Watanzania wachache wa kizazi kipya wanatambua mchango wa baadhi ya Watanzania wenye asili ya Kiasia kwenye harakati za kudai uhuru wa Tanganyika. Mmoja wa wanaharakati hawa ni Urmila Jhaveri ambaye hivi karibuni alitembelea Butiama.
Mama Urmila Jhaveri akiwa Butiama kwenye Makumbusho ya Mwalimu J.K. Nyerere. 
Mama Jhaveri, mwenye umri wa miaka 83 na ambaye alizaliwa kwenye kisiwa cha Pemba, ni mjane wa Kantilal Jhaveri aliyekuwa miongoni mwa wanasheria watatu wa upande wa utetezi kwenye kesi ya kashfa ya jinai ya mwaka 1958 iliyomkabili Mwalimu Julius Kambarage Nyerere wakati wa harakati za kudai uhuru iliyofunguliwa dhidi yake na serikali ya kikoloni ya Uingereza. Kantilal Jhaveri alifariki nchini India Januari 2014.

Wakati wa kudai uhuru wakati mume wake akiwa mmoja wa viongozi wa chama cha Waasia, Indian Association, kilichoshirikiana na kuunga mkono sera za Tanganyika African National Union (TANU), Urmila alishiriki kwenye harakati hizo akiwa mwanachama wa kitengo cha wanawake cha TANU ambacho kilijulikana kama TANU Women's Section.

Hivi karibuni amechapisha kitabu juu ya maisha yake kiitwacho Dancing with Destiny ambacho atakizindua tarehe 19 Julai  2014 jijini Dar es Salaam.

Itakuwa fursa nzuri kwa wote kukumbuka mchango muhimu wa makundi mbali mbali ya Watanzania kwenye harakati za kudai uhuru.

No comments: