Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Tuesday, October 14, 2014

Huduma kwa mteja mkoani Mara

Hili ni tukio la kweli na nimelishuhudia.

Siku moja nilikuwa abiria kutoka Nyamisisi kwenda Mwanza ndani ya basi lililoanza safari yake Tarime.

Baada ya muda kondakta alimsogelea abiria aliyekaa karibu yangu na mazungumzo yakawa hivi:

Konda: Nipe hizo hela!
Abiria: Ngapi?
Konda: Kwani hujui?!?!?!

Baada ya muda abiria akatoa nauli kamili halafu wakaendelea:

Abiria: Nifahamishe nauli sahihi kwa ustaarabu.
Konda: Kwani wewe nani? Usiniletee mambo yenu ya Kikurya!

Sehemu nyingine Tanzania watu wangekunjiana ngumi. Mkoa wa Mara ni mazungumzo ya kawaida tu kati ya mtoa huduma na mteja wake.

No comments: