Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Tuesday, July 14, 2015

Kwenye mchakato huu, dozi ya politiki ilizidi kiwango

Nafikiri ni General Defao aliyeimba: "umekalia politiki tu, kazi hufanyi". Katika kipindi ambacho Chama cha Mapinduzi (CCM) kimekuwa kikiendelea na mchakato wa kupata mgombea urais kwenye uchaguzi mkuu mwaka huu, hali hiyo ya kukalia politiki tu imekuwa kweli kwa watu wengi.

Wengi tunatambua umuhimu wa mchakato wowote wa kisiasa kama jambo muhimu katika jamii na jambo la msingi ni kupata viongozi wanaosimama kuwakilisha matakwa ya wengi. Na bila shaka ni suala ambalo kila mmoja wetu anapaswa kulifuatilia kwa karibu sana.

Lakini mchakato huo unapotufanya tuache kila kitu, hata zile kazi ambazo zinatulipa ajira, basi suala la siasa linakuwa limezidi dozi ya kawaida. Kuna watu wengi tu ambao hawakuwa na nafasi yoyote katika vikao vya maamuzi vya CCM vilivyokaa Dodoma kumpitisha John Magufuli ambao walienda Dodoma kufuatilia mchakato huo.

Baadhi ya ambao hatukuwa Dodoma tulikaa muda wote tukisikiliza taarifa kwenye vyombo vya habari kufuatilia mchakato. Wengine wengi walitumia muda wao kujibishana na wenzao kwenye mitandao ya jamii. Dozi haikuwa ndogo hata kidogo.
"I've always been and will continue to be a proud member of the ruling party CCM...I'm happy with all the five candidates and know that we'll get a great President to lead our beautiful nation...All the best....God Bless Tanzania󾍛....#ccm #chamachamapinduzi #januarymakamba #membe #magufuli #migiro #amina #umojaniushindi #tanzania"
Baadhi ya watia nia waliofikia hatua za mwisho za mchakato wa kupata mgombea urais wa CCM
Naamini watafiti wanaweza kubaini kushukua kwa uzalishaji katika kipindi cha majuma kadhaa yaliyopita.

Tushukuru kuwa mchakato huu wa CCM umeisha na labda watu watarejea kwenye maisha yao na majukumu yao ya kila siku.

No comments: