Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Wednesday, August 12, 2015

Lugha yetu Kiswahili: Kiswahili kinasambaa toka Scotland mpaka Butiama

Wanafunzi 12 toka Chuo Kikuu cha Edinburgh wapo kijijini Butiama kujifunza Kiswahili kwa mwezi mmoja.

Mafunzo yao ni sehemu ya mpango wa Chuo Kikuu cha Edinburgh kuvutia wanafunzi kutoka nje ya Scotland kujiunga na masomo mbalimbali katika chuo hicho maarufu, ambacho mmoja wa wanafunzi wake mashuhuri ni Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Wanafundishwa Kiswahili na walimu Watanzania watatu.
Wanafunzi kutoka Chuo Kikuu cha Edinburgh wakiwa Butiama, pamoja na walimu wao wa lugha ya Kiswahili.
Kuwepo kwa wanafunzi wa lugha ya Kiswahili kutoka Edinburgh hapa Butiama kwa Mwalimu Nyerere, ambaye pia anatambuliwa kama mmoja wa viongozi wa Tanzania ambao walitoa mchango mkubwa katika kukuza na kuendeleza lugha ya Kiswahili ni suala la fahari kubwa kwa mmoja wa waratibu wa mafunzo haya ya Kiswahili, Dk. Thomas Molony, ambaye mwaka jana alichapisha kitabu juu ya maisha ya Mwalimu Nyerere kinachoitwa Nyerere: The Early Years.

Akiwa Butiama wakati akifanya utafiti wa kitabu chake, nilipata fursa ya kuchangia kwa kiwango kidogo taarifa ambazo hatimaye alizitumia kwenye kitabu hicho.

Na mimi nakubaliana naye. Naamini kuwa Mwalimu Nyerere angekuwa hai angefurahi sana kushuhudia wanafunzi kutoka chuo chake cha zamani wakiwa Butiama kujifunza lugha ambayo yeye mwenyewe aliipenda na aliyoshiriki kuiimarisha.

No comments: