Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Thursday, September 10, 2015

Mada yangu ya leo: Hii siyo siasa

Tuawasikia baadhi ya viongozi waandamizi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wakimtaka mgombea urais wa UKAWA akubali wakutane kwenye mdahalo ili waeleze maovu yake. Yeye anasema kama wana ushahidi kuhusu maovu yake waende mahakamani. Hii siyo siasa.

Nionavyo mimi, siasa ingekuwa hivi:

1. Kama una tuhuma dhidi ya mgombea urais husubiri awe rais kwanza. Unasema yale unayoyafahamu. Akisha kuwa rais halafu utafanya nini? Utaomba mdahalo?

2. Mpiga kura ana haki ya kufahamu taarifa zote muhimu juu ya wagombea kabla hajafikia uamuzi wa kumchagua yule ambaye anaona anafaa. Kuamua kuwa taarifa hizo ni kama mali adimu haina tofauti na kujifanya mtaalamu wa bishara (au taaluma nyingine) ambaye ametumia muda mwingi kupata elimu na uzoefu kwenye taaluma yake halafu anaamua, kwa haki kabisa, kuwa taarifa hizo hazitoki mpaka kwa masharti yanayomnufaisha yeye, au kwa pesa au kwa njia nyingine atakayoamua. Ni wajibu wa kiongozi yoyote makini kumpa mpiga kura taarifa sahihi, hasa wakati wa uchaguzi.

3. Mpaka sasa, tumemsikia mtuhumiwa akisema kuwa hana tuhuma yoyote na, kwa mantiki hiyo, anaposema nendeni mahakamani ni sawa kabisa. Wale wenye taarifa hizo wakaziibue mahakamani. Watuhumiwa wachache sana hukubali kosa nje ya mahakama.

Kwa hayo machache, sisemi kuwa tuhuma ni za uongo.

Ninachoona ni kundi moja ambalo limekosa ujasiri wa kutamka wanalotaka kutamka na badala yake kuwafanya wapiga kura kubaki wanabishana wenyewe kwa wenyewe na ujinga wao* (kama ujinga huo upo kweli) bila kuwapa taarifa ambazo zinaweza kuwasaidia kufanya chaguo sahihi.

Kama huo ujasiri unakosekana, basi ni bora kunyamaza tu. Kuwafanya wapiga kura kuwa wajinga mara ya pili ni hatari kisiasa.

Huo ndiyo ujumbe wango leo hii.

*Wale ambao mtakimbilia kwenye Tume ya Mawasiliano kunilalamikia kuhusu kutumia neno "ujinga" ni kwamba siyo tusi, ni hali ya kutofahamu tu.

No comments: