Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Tuesday, December 1, 2015

Kufanikisha falsafa ya Sasa Kazi tu! ni kazi kweli kweli!

Tunajifunza mengi kwa kusikiliza. Leo nimemsikiliza mama wa kijijini Butiama akilalamika kwangu tena kuhusu binti yake kuondoka nyumbani na kuhamia kwa mtu aliyezaa naye.

Tatizo ni kuwa binti mwenyewe ana umri wa miaka 15 tu, na aliyempa ujauzito ni mtu mzima. Alimpa hiyo mimba binti akiwa shuleni, na kwa mujibu wa sheria zilizopo angestahili kuchukuliwa hatua za kisheria. Hayo hayakutokea.

Nahisi hayakutokea kwa sababu mama wa binti, badala ya kupeleka hilo suala mbele ya sheria, alifikia makubaliano na huyo jamaa na inawezekana kuwa alikuwa anapewa pesa ili kutulia.

Sasa leo kalalamika tena kuwa binti karudi kule kule na akaniambia kuwa sasa anakusudia kufikisha suala hilo polisi. Lakini njia anayotumia haijanyooka vizuri. Kaniambia kuwa ana jirani yake polisi ambaye amemuomba aende kumkamatia yule mhalifu.

Jirani yake kakubali lakini amemwambia ampe shilingi elfu kumi ili amfanyie hiyo kazi. Yeye alisema hana hizo pesa, na akamwambia yule jirani kuwa amfanyie tu hiyo kazi kwa kuwa wanahusiana pia kiukoo. Jirani polisi hakusumbuliwa sana na hoja ya uhusiano wa kiukoo, na amemwambia mlalamikaji atafute angalau shilingi elfu tano ili afanye hiyo kazi.
 
Rais John Magufuli (wa pili kutoka kushoto), akiwa na marais wastaafu (kutoka kushoto kwenda kulia) Ali Hassan Mwinyi, Jakaya Mrisho Kikwete, na Benjamini William Mkapa. (Picha kwa hisani ya CCM Blog)

Miongoni mwa vielelezo kuwa uongozi ni kazi kubwa ni pamoja na tukio hili. Kwenye ngazi hii ya chini, kujenga imani kuwa falsafa ya Sasa Kazi tu! itafanikiwa ili mradi yupo rais na waziri mkuu wachapa kazi ni ndoto tu. Mabadiliko chanya yatapatikana iwapo wote tutashiriki kwa namna tunavyoweza kuleta mafanikio tunayotarajia.

2 comments:

Seleman said...

good post

Ngara IT Solutions said...

Kusema kweli miongoni mwa vitu vitakavyokwamisha falsafa hii ni pamoja na jamii kudhania kuwa hii inawahusu watumishi WA serikali peke yao. Lakini pia wakuu WA idara kutumia mwanya huo kupenyeza chuki zao binafsi na watumishi walioko chini yao na kuwanyanyasa.