Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Friday, November 9, 2018

Leo ni kumbukumbu ya harusi ya Milton Obote na Maria Kalule

Siku kama ya leo, miaka 55 iliyopita, Apollo Milton Obote, Waziri Mkuu wa Uganda alifunga ndoa na Bi Maria Kalule kwenye sherehe iliyohudhuriwa na wageni 20,000.

Bibi harusi alikuwa ni katibu muhtasi kwenye ubalozi wa Uganda kwenye Umoja wa Mataifa, jijini New York.

Harusi yao ilifungwa na Askofu wa Uganda, Dk. Leslie Brown kwenye Kanisa la Namirembe. Wakati wa ibada ya ndoa, Askofu alimwambia Bi Kalule:

“Hufungi ndoa na Waziri Mkuu. Unafunga ndoa na mtu unayempenda. Lakini kwa sababu yeye pia ni Waziri Mkuu basi ndoa hii ina umuhimu mkubwa kwa maisha ya taifa la Uganda.”

Maharusi walipokuwa wanaondoka kanisani mamia kadhaa ya waliohudhuria walishuhudia wakielekea kwenye sherehe iliyofanyika kwenye uwanja wa Michezo wa Lugogo, sehemu pia zilipofanyika sherehe za uhuru Oktoba 1962 wakati Uganda ilipopata uhuru wake.


Jomo Kenyatta na Jaramogi Oginga Odinga ni miongoni mwa waalikwa waliohudhuria kutoka Kenya.


Baadaye usiku huo, maharusi walisafiri kutoka Entebbe kuelekea London kuelekea kwenye fungate yao.

No comments: