Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Tuesday, May 11, 2010

Barabara ya zamani ya Mwanza

Siku moja nikiwa ndani ya basi kutoka Arusha kuja Butiama ulizuka ubishi mkali wa kisiasa kati ya abiria na dereva wa basi kuhusu iwapo Chama cha Mapinduzi (CCM) kimeleta maendeleo yoyote nchini tangu kuondoka wakoloni. Abiria wawili kina mama walisema hakuna maendeleo yoyote, wakati dereva wa basi alisema yapo maendeleo.

Siku hiyo basi liliwahi kufika Mugumu, kituo kimojawapo katika safari ya kuelekea Musoma, na wale abiria wakasema kuwa tulikuwa tumewahi sana kufika kwa kuwa barabara ilikuwa nzuri wakilinganisha na hali ya barabara ilivyokuwa vipindi vya nyuma. Niliwakumbusha kuwa usemi kuwa CCM haijaleta maendeleo itaonekana kutokuwa na nguvu kwa wao kusifia kuwa barabara ilikuwa nzuri kuliko zamani.

Labda ukweli ni kuwa serikali yoyote ambayo ingekuwa madarakani baada ya uhuru ingelazimika kujenga barabara sehemu mbalimbali za Tanzania.

Barabara mojawapo ambayo imebadilika sana kwa sasa ni ile ya Mwanza hadi Musoma. Nakumbuka kuwa barabara ya zamani ilipita Butiama, na likuwa ni barabara ya vumbi ambayo


hii leo (pichani, juu) bado inatumika kwa safari za gari kwenda Arusha kupitia mbuga za Serengeti na Ngorongoro. Barabara hiyo ilikuwa ikichepukia Nyamuswa kuelekea Bunda na Mwanza.

Kati ya mwaka 1977 na 1983 Serikali ilijenga barabara mpya ya lami ambayo haukupita tena Butiama, lakini ikasogezwa kiasi cha kilomita 11 mashariki ya Butiama na sasa inapita karibu na mji wa Kiabakari.

Hata hivyo barabara hiyo ilikamilika na kasoro kidogo. Daraja mojawapo lililoopo karibu na kijiji cha Sabasaba halina upana ule ule wa barabara na gari zinapokutana hapo, hasa zikiwa gari
kubwa, haziwezi kupishana katikati ya daraja na inabidi dereva kutoa nafasi kwa dereva mwenzake apite.
Picha: Kasoro kwenye barabara ya Mwanza hadi Musoma, daraja jembamba.

No comments: