Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Thursday, June 10, 2010

Balozi mpya wa Tanzania Afrika ya Kusini

Balozi mpya anayewakilisha Tanzania nchini Afrika ya Kusini, Mhe. Radhia Msuya, hivi karibuni aliwasilisha hati za utambulisho kwa Rais Jacob Zuma wa Afrika ya Kusini mjini Pretoria.

Picha: Rais Zuma (katikati), na Balozi Msuya (kulia)

Utambulisho huo ulifanyika tarehe 8 Juni 2010 kwenye Makazi ya Rais yaliyopo jijini Pretoria. Rais Jakaya Kikwete alimteua Balozi Musya mwezi Machi mwaka huu kushika nafasi iliyoachwa wazi na Balozi Emmanuel Mwambulukutu aliyestaafu. Kabla ya uteuzi wake Balozi Msuya aliongoza Idara ya Ulaya na Amerika kwenye Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

Picha (kutoka kushoto kwenda kulia): Robert Kahendaguza (Mkuu wa Utawala na Fedha wa Ubalozi wa Tanzania), Rais Zuma, Balozi Msuya, na Brigedia Jenerali Simon Mumwi (Mwambata Jeshi, Ubalozi wa Tanzania)

No comments: