Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Monday, November 1, 2010

Vincent Nyerere wa CHADEMA ashinda ubunge Musoma Mjini

Taarifa rasmi iliyotangazwa na msimamizi wa uchaguzi wa Musoma Mjini, saa 11:30 alfajiri hii, imethibitisha ushindi wa Vincent Nyerere wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kuwa mbunge mpya baada ya kumshinda aliyekuwa mbunge, Vedasto Mathayo Manyinyi wa Chama cha Mapinduzi (CCM).
Vincent Nyerere, mbunge mteule wa jimbo la Musoma Mjini, akihutubia mkutano wa uchaguzi uliyofanyika Musoma wakati wa kampeni za uchaguzi za zilizoisha juzi.
Matokeo rasmi ni haya:

Jina la Mgombea
Chama
Kura  Alizopata
Asilimia ya Kura
Zote Zilizopigwa
Vincent K. Nyerere
CHADEMA
              21,225
                   59.71
Vedasto  M. Manyinyi
CCM
              14,072
                   39.38
Mustapha J. Wandwi
CUF
                   253
                     0.71
Chrisant N. Nyakitita
DP
                     53
                     0.15
Tabu S. Machibya
NCCR - Mageuzi
                     19
                     0.05

1 comment:

Subi Nukta said...

Kaka, asante sana kwa taarifa za majibu haya.