Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Sunday, December 5, 2010

Jaffar Amin amewasili Moshi kupanda Mlima Kilimanjaro

Bwana Jaffar Amin amewasili Moshi leo mchana tayari kwa kushiriki nami kupanda Mlima Kilimanjaro kwa madhumuni ya kuchangisha pesa za hisani kwa ajili ya Sekondari ya Wasichana ya Chief Wanzagi ya mkoani Mara, pamoja na kuchangia asasi ya mjini Buoka inayoitwa BUDAP inayojishughulisha na miradi ya kusaidia walemavu kwa njia ya mafunzo na ajira.
Jaffar Amin, pichani, mara baada ya kuwasili Moshi mjini leo mchana, akiwa na hamasa kubwa ya kupambana na Mlima Kilimanjaro ambao unaonekana nyuma yake.
Baada ya kumpokea katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro, Jaffar alisema amejitayarisha vyema kupanda Mlima Kilimanjaro kuanzia Jumanne, 7 Desemba 2010 kwa muda wa siku nane.

Ni mara yangu ya tatu kupanda huo mlima, na mara ya kwanza kwa Jaffar. Matarajio na maombi kwa wadau mbalimbali ni kuchangia mojawapo ya walengwa wa tukio hili ambalo linajulikana kama The Mwalimu Nyerere/Mt. Kilimanjaro Charity Climb 2010.

Tafadhali changia mojawapo ya hawa wafuatao (au wote):

Jina la Akaunti:
Chief Edward Wanzagi Girls' Secondary School Fundraising

Benki:
National Bank of Commerce, Tawi la Musoma

Namba ya Akaunti:
030201191529

Pamoja na:

Jina la Akaunti:
Budap

Benki:
National Bank of Commerce, Tawi la Bukoba

Namba ya Akaunti:
027201092625
##################################

No comments: