Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Thursday, October 27, 2011

Waziri Mary Nagu azindua ofisi ya kituo cha uekezaji Mbeya


Taarifa zifuatazo zimetolewa na blogu ya Mbeya Yetu:

Waziri Mary Nagu amezindu ofisi ya kanda ya Kituo cha Uwekezaji mjini Mbeya juma liliopita.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwezeshaji na Uwekezaji), Dk. Mary Nagu akikata utepe kuzindua ofisi ya kituo cha uwekezaji (TCI) nyanda za juu kusini mjini Mbeya.
Akizindua ofisi hiyo mwishoni mwa wiki jijini Mbeya, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwezeshaji na Uwekezaji), Dk. Mary Nagu alisema ofisi hiyo ni muhimu katika kusaidia wajasiriamali na wawekezaji wa mikoa ya Ruvuma, Iringa Rukwa na Mbeya kuitumia kwa ajili ya kuanzisha miradi mbalimbali ya uwekezaji.

Ufunguzi huo pia ulihudhuriwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Kituo cha Uwekezaji, Balozi Elly Mtango, Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Raymond  Mbilinyi, Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, Abbas Kandoro.

No comments: