Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Wednesday, January 4, 2012

Maoni ya Amani Millanga kuhusu mafuriko ya Dar: sehemu ya nne kati ya nne

Maoni ya Amani Millanga kuhusu mafuriko ya Dar: sehemu ya nne kati ya nne

Funzo
Mafuriko haya yanatupa funzo la kuhakikisha kuwa tunavyo vyombo na vifaa vya kukabiliana na hali kama hii isitokee siku nyingine. Lakini pia tunakuwa wepesi wa kuchukua hatua za kuokoa maisha ya watu na si kusubiri hali inapokuwa mbaya ndipo tunaleta msaada kwa watu. Maisha ya watu wengi yangepotea kama si hatua za haraka na za makusudi zilizofanywa na mbunge wa Mafia za kukodi boti na kuipeleka eneo la mafuriko. Vyombo vya uokozi vya serikali vilikuwa wapi?

Miaka 50 ya Uhuru, changamoto bado ni nyingi na kubwa sana lakini la kusikitisha zaidi ni kwamba mafunzo ya kuthamini utu wa watu ambayo tuliyarithi kutoka kwa hayati Baba Mwalimu Julius Kambarage Nyerere yametoweka katika nyoyo zetu na leo hii tunasisitiza waathirika "wahame" tena bila fidia. Tumewaona wanawake wajawazito na watoto wakiwa hawana chakula; tumewaona majeruhi hawapati matibabu katika muda muafaka; tumewaona wazee hawana nguo za kujisitiri. Ndugu zangu Watanzania, ama kwa hakika tumeuona umaskini ukitembea. Ni uchungu ulioje.

Mungu Ibariki Tanzania

No comments: