Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Friday, January 27, 2012

TPBC yaingia makubaliano na Chuo cha Polisi Moshi

Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBC) na Chuo cha Polisi cha Kimataifa cha Moshi (CCP) wameingia makubaliano ya kukuza na kuendeleza vipaji vya michezo vya vijana.

Katika Makubaliano hayo yaliyofikiwa mwezi August, 2011, TPBC na CCP watashirikiana kuchagua vijana wenye vipaji vya mchezo wa ngumi na kuwaendeleza ili waweze kucheza michezo ya majeshi pamoja na mashindano mengine ndani na nje ya Tanzania.

Makubaliano haya yamekuja wakati ambapo Tanzania inahitaji msukumo mkubwa kwenye medani ya michezo ili kuweza kufufua ari na moyo wa michezo kama ilivyokuwa katika miaka ya 70 na 80.

Aidha, Makubaliano haya yana lengo la kuandaa jeshi zuri la wanamichezo hodari watakaoleta sifa jeshi la Polisi pamoja na Tanzania kwa ujumla. Tayari vijana wengi wanafanya mazoezi katika kambi (Gym) ya ngumi ambayo imewekwa katika viwanja vya michezo vya CCP. Kambi hiyo inawashirikisha pia vijana kutoka maeneo mengine mkoani Kilimanjaro ambao sio Polisi.

Katika kusimamia hili, Rais wa TPBC Onesmo Ngowi akishirikiana na Afisa Mipango na Utawala wa CCP Superintendent of Police, Lutusyo Mwakyusa watahakikisha kuwa vifaa muhimu vinapatikana pamoja na mazingira ya kufanyika mazoezi na upatikanaji wa wataalam wanaotakiwa wanapatikana.

Naye Superintendent of Police, Yahya Mdogo ambaye ni Afisa wa Michezo katika Chuo cha Polisi cha Kimataifa Moshi ataangalia kwa karibu mwendendo mzima wa mahitaji ya kila siku ya mazoezi.

Tayari TPBC imeshatoa vifaa muhimu vya mazoezi pamoja na wataalam (Makocha) wa kuwafundisha mabondia hao wako katika sehemu ya mazoezi.  Vijana wengi ambao walikuwa hawana kazi au mahala pa kwenda wakati wa saa za jioni kwa sasa wanafanya mazoezi na wenzao katika uwanja wa CCP.

Aidha, baadhi ya mabondia kutoka katika mkoa wa Kilimanjaro ambao walikuwa wameweka kambi katika jiji la Nairobi nchini Kenya na Arusha wamejumuika katika kambi hii mpya. Mabondia hao ni pamoja na Pascal Bruno anayejulikana na wengi kama "Prince Kilimanjaro", Emilio Norfat, Charles Damas, Alibaba Ramadhani, Robert Mrosso, Bernard Simon na wengine wengi

Baadhi ya wataalam waliojitokeza kuwafundisha vijana hawa ni pamoja na Felix Joseph na Pius Msele ambao kwa nyakati tofauti wamewahi kuwa wachezaji na makocha wa timu ya ngumi ya taifa.

Makubaliano haya ni baadhi tu ya mikakati mipya za TPBC za kuamsha ari ya mchezo wa ngumi kwa kuzisambaza mikoani kuliko ilivyozoeleka ngumi kufanyika katika mkoa wa Dar -Es-Salaam peke yake.

"Kwa sasa kazi kubwa tulivyo nayo ni kuzipeleka ngumi mikoani ambako tunaamini kuna vijana wengi sana wenye moyo pamoja na vipaji vikubwa" alisema Ngowi.

No comments: