Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Tuesday, February 21, 2012

Salim Mkalekwa kupambana na Abdallah Mohamed (Prince Naseem)

Bingwa wa ndondi za kelipwa wa walterweight (kilo 67) wa Pugilistic Syndicate of Tanzania (PST), Abdallah "Prince Naseem" Mohamed, anatarajia kupanda ulingoni tarehe 24 Februari 2012, katika pambano la ubingwa dhidi ya bondia Salehe Mkalekwa.
Bondia Salehe Mkalekwa (kushoto), mratibu wa pambano Shabani "Mwayamwaya" Adiosi (katikati), na bondia Abdallah "Prince Naseem" Mohamed (kulia).
Mapambano ya utangulizi yatawahusisha mabondia Shaaban Zungu dhidi ya Hassan Debe (kilo 55); Safari Mbeyu dhidi ya Ibrahim Maokolo (kilo 67); Geoffrey Pacho dhidi ya Dickson Kawiani, na Kulwa Kindondi dhidi ya Khaji Hamisi. Uzito wa mabondia katika mapambano haya mawili ya mwisho haukupatikana.

Pambano hilo linaratibiwa na Shabani "Mwayamwaya" Adiosi na litafanyika kwenye ukumbi wa New Kibeta, Mbagala Kuu, Dar es Salaam.

Picha na taarifa kwa hisani ya Super D Boxing Coach.

No comments: