Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Friday, February 3, 2012

Francis Cheka amshinda Karama Nyilawila kwa pointi

Katika pambano lililofanyika kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro tarehe 28 Januari 2012 bondia Francis Cheka alimshinda Karama Nyilawila kwa pointi katika pambano la uzito wa "Super Middleweight" lisilokuwa la ubingwa.

Katika pambano hilo kali mabondia wote wawili walitupiana makonde ya kujibizana lakini kwa mujibu wa majaji wa mchezo huo, Cheka aliibuka mshindi. Majaji walitoa pointi zifuatazo: John Chagu 100 - 96, Mark Hatia 96 - 97, na Boniface Wambura 99 - 97. Refa wa mchezo alikuwa Nemes Kavishe.
Karama Nyilawila (kushoto) akiinama kukwepa kombora la Francis Cheka katika pambano la hivi karibuni liliofanyika kwenye Uwanja wa Jamhuri, Morogoro. (Picha kwa hisani ya superboxingcoach)
Pambano hilo lilisimamiwa na Kamisheni ya Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBC), na promota wa pambano alikuwa Philemon Kyando.

No comments: