Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Wednesday, February 29, 2012

Wizi wa mitihani ni janga la Taifa

Picha hii (hapa chini) ni ya tangazo lililobandikwa kwenye chuo kimojawapo mashuhuri cha Tanzania kwenye moja ya majiji ya Tanzania.
Nimefuta majina ya walioorodheshwa ili kuhifadhi majina ya wahusika.

Tangazo linaashiria kuwa walioorodheshwa wanatuhumiwa kuibia kwenye mitihani. Mwalimu mmoja ambaye alizisikia taarifa hizi alisema kuwa anaamini kuwa hawa walionaswa ni asilimia ndogo sana ikilinganishwa na wale ambao waliibia lakini hawakunaswa, ambao baada ya muda watahitimu masomo yao.

Kwa nini wizi wa mitihani ni janga la Taifa? Mwalimu Nyerere, katika moja ya hotuba zake, alisema:
"...[shabaha ya elimu ni] kurithisha kutoka kizazi kimoja had kizazi kingine maarifa na mila za taifa, na kuwaandaa vijana wawe tayari kuchukua nafasi zao katika kulitumikia na kuliendeleza taifa."
Kwa mtindo huu, tunarithisha majukumu ya kulitumikia na kuliendeleza taifa kwa wahitimu ambao hawana elimu inayolingana na shahada wanazotoka nazo vyuoni. Ni sawa sawa na kujenga nyumba kwenye msingi hafifu. Kuna siku moja nyumba itaporomoka na tutajikuta tunaongozwa na watu wa mataifa mengine ambapo ipo elimu ya kweli, na wako wasomi wa kweli.

Kuna mtaalamu mmoja anasema kuwa tayari tunaongozwa na watu hao.

posted from Bloggeroid

No comments: