Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Saturday, September 14, 2013

Asikwambie mtu, Mtanzania mwenye simu siyo maskini

Baadhi ya matumizi ya simu yanaashiria kuwa Watanzania wanao uwezo mkubwa.

Nimekuwa msikilizaji wa mazungumzo ya simu ninapokuwa mitaani au safarini na katika utafiti usiyo rasmi ambao nimefanya, watu wengi wanaotumia simu hawazitumii kama nyenzo za kuongeza ufanisi katika shughuli zao, bali huzitumia kama chombo cha kupiga porojo zisizo na manufaa kwao au kwa wanaoongea nao.

Sina mamlaka kuhoji ambavyo mtu aliye huru anaamuaje kutumia salio lako kwenye simu, lakini kukosa mamlaka hayo hakufuti ukweli kuwa Watanzania wengi tunapoteza pesa zetu za mawasiliano kupiga porojo na kutuma ujumbe wa maandishi ambao hauleti maendeleo yoyote kwetu na kwa Taifa. Wanaochekelea ni wamiliki wa kampuni za simu ambao bila shaka wanatunisha mifuko yao kwa kila sekunde inayopita.

Chukua mfano huu: nimeketi ndani ya ndege iliyowasili kwenye uwanja wa ndege halafu abiria kadhaa wanawasha simu zao na kuwapigia simu watu ambao wamefika kuwapokea uwanjani wakiwaambia kuwa kuwa ndege imeshatua. Hii nimeshuhudia mara nyingi. "Vipi, umeshafika? Na sisi ndiyo tumetua."

Kwangu ingekuwa inaleta maana zaidi iwapo baada ya kutoka uwanjani na asimuone aliyempokea ndiyo apige simu kumuuliza kilichomsibu mwenyeji wake mpaka asifike uwanjani.

Siku za hivi karibuni nimeshuhudia mtu anayeongea kwenye simu karibu siku nzima. Akimaliza simu moja anapiga na kuongea na nyingine. Sijui anaongea nini kwa sababu anaongea Kizanaki (lugha ambayo siifahamu vizuri) lakini pamoja na kutofahamu lugha hiyo bado sipati picha ya suala ambalo litanifanya niongee kwa siku nzima. Hoja yangu hapa ni kuwa siyo rahisi kuongea mfululizo kwa karibu siku nzima na ukawa unapanga masuala ya kuleta maendeleo kwako au kwa jamii inayokuzunguka. Asilimia kubwa ya mazungumzo itakuwa porojo ambayo matokeo yake itakufanya kupungukiwa tu pesa ambazo ungeweza kuzitumia kwa jambo la maana zaaidi na lenye manufaa. Dakika chache kwenye simu kila siku zinafikia pesa nyingi baada ya muda mrefu.

Naweza kuwa nitatofautiana na wengi lakini ule woga wa serikali hivi karibuni kutoza shiling elfu moja kwa mwezi kwa kila mtumiaji wa simu ulikuwa woga wa kisiasa kwa sababu baadhi ya makundi ya jamii yalilivalia njuga suala hilo na kodi hiyo ya mawasiliano ilionekana kuwa ingeipunguzia serikali ushawishi kwa Watanzania. Inawezekana kuwa serikali inayo matatizo mengi 

Ukweli ni kuwa watumiaji wengi wa simu wanatumia pesa nyingi kwa mwezi kuongea na kuandika ujumbe wa maandishi usiyo na manufaa yoyote lakini ambao unawagharimu kiasi kikubwa kuliko hiyo shilingi elfu moja.

No comments: