Mimi niliamini kuwa wale wanaanga wawili walifika kwenye mwezi. Sijui kwa sababu ipi sikuwaza kuwa ni uongo, lakini nakumbuka tu kuwa niliamini taarifa tulizosikia na kusoma bila kuhoji. Kwa umri wetu maoni yetu, ya kuamini au kutoamini, hayakutokana na ushahidi wowote tuliokuwa nao lakini ajabu ni kuwa tulikuwa na maoni tofauti.
![]() |
Mwanaanga Edwin "Buzz" E. Adrin akionekana kwenye mwezi pembeni ya chombo kilichotua kwenye mwezi tarehe 20 Julai 1969. Picha ya National Space Agency (NASA). |
Niligundua hivi karibuni kuwa wasiwasi wa taarifa zile kwa Richard za mwaka 1969 haukutokea Tanzania tu; hata baadhi ya Wamarekani hadi hii leo hawaamini kuwa Wamarekani wenzao walifika kwenye mwezi na wanasema kuwa mandhari ya mwezi ambayo tunaiona kwenye baadhi ya picha ilibuniwa na kutengenezwa hapa hapa duniani kwenye jengo moja kubwa linalohifadhi ndege kwenye uwanja mmojawapo wa ndege wa nchini Marekani.
Inawezekana kuwa tofauti ya sasa na mwaka 1969 ni kuwa watu wengi zaidi wamejenga desturi ya kutoamini taarifa za serikali na mamlaka mbalimbali. Serikali na mamlaka zimebainika mara nyingi kutoa taarifa za uongo na watu sasa wanaposikia taarifa hizo huanza kwa kutoamini hizo taarifa mpaka pale watakapopata taarifa kutoka vyanzo tofauti zinazothibitisha ukweli wa hizo taarifa za awali.
Taarifa inayofanana na hii:
http://muhunda.blogspot.com/2012/01/ingekuwa-unaishi-kwenye-sayari-ya.html
Taarifa inayofanana na hii:
http://muhunda.blogspot.com/2012/01/ingekuwa-unaishi-kwenye-sayari-ya.html
No comments:
Post a Comment