Baada ya kutangazwa Azimio la Arusha, mwaka 1967, baadhi ya makundi ya Watanzania kutoka maeneo mbalimbali ya Tanzania yalianza kutembea kwa mguu kutoka sehemu moja hadi nyingine ya nchi kuunga mkono Azimio la Arusha.
 |
Picha ya Idara ya Habari Maelezo |
Kwenye picha ni vijana kutoka mkoa wa Mara ambao walitembea hadi Dar es Salaam kuunga mkono sera ambayo iliweka umuhimu kwa serikali kumiliki njia kuu za uchumi na kutumia rasilimali ya Taifa kwa manufaa ya wananchi.
Ikulu, Dar es Salaam, walipokelewa na Rais Mwalimu Julius Kambarage Nyerere.
No comments:
Post a Comment