Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Friday, March 23, 2018

Ukitaka kula usiende jikoni

Nina desturi ya kununua mahindi ya kuchoma yanayouzwa mitaani. Nilichoshuhudia miezi kadhaa iliyopita kimenipunguzia hamu ya kula tena mahindi hayo.

Nilisogelea mchoma mahindi na kuchagua mhindi uliyokuwa tayari juu ya jiko la mkaa. Baadaye kidogo, mmoja wa mahindi aliyokuwa akichoma ulianguka chini na kuseleleka mbali na alipokaa.

Alimtuma mwanae kuuokota chini na akaurudisha jikoni kuendelea kuuchoma baada ya kuufuta mchanga. Haukuwa ule mhindi niliyouchagua mimi ila nilitambua kuwa muda si mrefu atafika mteja kama mimi na kulishwa mhindi huo na, bila shaka, kuambukizwa minyoo.

Lakini haikuwa hatari ya kupata minyoo tu. Mchoma mahindi alikuwa na kikohozi. Na kila alipokohoa aliziba mdomo akitumia mkono wake wa kulia, ikiwa ni tabia ile ambayo baadhi wamefundishwa ili kuwakinga wengine kuathirika na athari za maambukizo yanayoweza kusambazwa na anayekohoa.

Tatizo ni kuwa ni mkono huo huo aliutumia kugeuzia mahindi aliyokuwa anachomea wateja, pamoja na langu. Mkono ulikuwa unatoka mdomoni na kushika mhindi.

Aliponiambia mhindi wangu umeiva, badala ya kuanza kula pale pale kama ilivyokuwa desturi yangu, nikamuomba aufunge vizuri nikaondoka nao lakini sikuula na ndiyo ikawa mwisho wa kununua mahindi ya njiani.

Labda kwa sababu nimeanza kulima mahindi nitakuwa nachoma mahindi ninayovuna shambani kwangu.

Nimewahi kusikia msemo kuwa ukitaka kula chakula cha mgahawa usiingie jikoni. Utakayoyaona huko yatakatisha njaa yako.

No comments: