Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Tuesday, April 27, 2010

Kumbukumbu ya Karume

Mapema mwezi huu Katibu Mkuu wa chama cha Wananchi (CUF) Seif Shariff Hamad alihudhuria khitma ya Marehemu Rais Abeid Karume, aliyeuwawa tareke 7 Aprili 1972.

Picha mbili za juu: Kaburi la Marehemu Sheikh Abeid Amani Karume aliyezikwa makao makuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Kisiwandui, Zanzibar.

Khitma hiyo iliyofanyika kwenye makao makuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Kisiwandui, Zanzibar, na ambayo ilikuwa ni sehemu ya maadhimisho ya siku ya Karume inayoadhimishwa tarehe 7 Aprili kila mwaka, ilihudhuriwa na viongozi wakuu wa Tanzania ikiwa ni pamoja na Rais Jakaya Kikwete, Rais Amani Karume wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Makamu wa Rais Dk. Mohamed Shein, pamoja na Waziri Kiongozi wa Zanzibar Shamsi Vuai Nahodha.

Kabla na baada ya khitma nilishuhudia Maalim Seif akiongea kwa uchangamfu na viongozi wenzake waliyohudhuria (sehemu kubwa ya vingozi hao ikiwa ni viongozi wa CCM), kitendo ambacho kingeonekana cha kawaida kwa mgeni wa siasa za miaka ya hivi karibuni zilizosheheni uhasama mkubwa kati ya viongozi na wanachama wa CCM na CUF.

Hakikuwa kitendo cha kawaida na vichwa vya habari kuhusu siku hiyo vilizungumzia kitendo hicho cha kihistoria na ambacho kinaonekana kuashiria kufungua ukurasa mpya wa maridhiano kati ya CCM na CUF kwa upande wa Zanzibar.

Jitihada za hivi karibuni za Rais Aman Karume na za Maalim Seif kutafuta suluhu ya kipindi kirefu cha kutoelewana kati ya CCM na CUF, pamoja na jitihada za awali za kutafuta muafaka, zitaonekana kuwa ndiyo chimbuko la Maalim Seif kuonekana kwenye mkusanyiko ambao zamani ungeonekana kuwa ni wa wana CCM tu. Leo hii, Baraza la Wawakilishi limesharidhia uundwaji wa serikali ya mseto kwa Zanzibar, jambo ambalo linaweza kupunguza uhasama na kuimarisha maridhiano.

Picha: Baada ya shughuli rasmi Maalim Seif 'alivamiwa' na waandishi wa habari na kujibu maswali kadhaa.

No comments: