Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Monday, December 20, 2010

Mchango wa kwanza wa hisani umepatikana kwa Sekondari ya Wasichana ya Chief Edward Wanzagi

Mchango wa kwanza wa thamani ya Sh.500,000/- (laki tano) kuchangia jitihada za The Mwalimu Nyerere/Mt. Kilimanjaro Charity Climb 2010 kusaidia Shule ya Sekondari ya Chief Edward Wanzagi umetolewa na Tanzania Gatsby Trust.

Shukurani za dhati ziende kwa Tanzania Gatsby Trust (TGT), na kwa Afisa Mtendaji Mkuu wa TGT, Mama Olive Luena.

Unayesoma habari hizi unaombwa kuchangia mojawapo ya walengwa wafuatao wawili wa mwaka huu (au walengwa wote wawili):

Jina la Akaunti:
Chief Edward Wanzagi Girls' Secondary School Fundraising

Benki:
National Bank of Commerce, Tawi la Musoma

Namba ya Akaunti:
030201191529

Pamoja na:

Jina la Akaunti:
Budap

Benki:
National Bank of Commerce, Tawi la Bukoba

Namba ya Akaunti:
027201092625

Sunday, December 19, 2010

Masahihisho kwenye namba ya akaunti ya BUDAP

Nilifanya makosa katika taarifa ya awali niliyotoa juu ya namba ya akaunti ya Budap, mmoja wa walengwa wa The Mwalimu Nyerere/Mt. Kilimanjaro Charity Climb iliyomalizika hivi karibuni mjini Moshi.
Juu ya kilele cha Mlima Kilimanjaro. Kulia unaonekana Mlima Meru.
Taarifa sahihi ni hizi:


Jina la Akaunti:
Budap

Benki:
National Bank of Commerce, Tawi la Bukoba

Namba ya Akaunti:
027201092625

Wednesday, December 15, 2010

CCM wafungua tawi Uingereza, CHADEMA juu ya Mlima Kilimanjaro

Taarifa zilizonifikia hivi punde zinaeleza kuwa baadhi ya Watanzania waishiyo katika mji wa Luton Uingereza walijumuika 12 Desemba 2010 kwa ajili ya ufunguzi wa tawi jipya katika mji wa Luton, ufunguzi uliyofanyika katika hoteli ya Chiltern UK.

Taarifa hiyo, kwa hisani ya Tawi la CCM Uingereza inaendelea:
Wengi wao wanasema wana imani kubwa na CCM katika kuiongoza Tanzania kwa kuonyesha muelekeo wa kuwa na imani na vijana wasomi wachapakazi waliyoko ndani na nje ya nchi.



Ufunguzi huo ambao uliongozwa na mwenyekiti wa tawi la CCM - UK, Maina Owino, kwa kushirikiana na viongozi wengine wa CCM akiwemo Katibu Mwenezi wa Siasa, Moses Katega. Pia viongozi kutoka mashina ya Reading, Birmingham na sehemu zote za London walijumuika.


Katika hotuba yake fupi Ndugu Maina Owino alitoa changamoto nyingi za mafanikio  yaliyopatikana katika kipindi cha miaka mitano iliyopita chini ya uongozi wa Mwenyekiti wa CCM Taifa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete katika nyanja mbalimbali kama madini, elimu, ukusanyaji wa mapato ya serikali, waajiriwa wenye sifa za kukidhi nafasi za uongozi serikalini katika nyanja zote, na ujasiriamali kwa Watanzania wanaojitafutia maendeleo bila bugudha.


Changamoto kuhusu ushiriki wa vijana wasomi hapa Uingereza kuingia katika mchakato wa siasa ndani ya Chama ili kuleta mabadiliko yatakayozidi kukiimarisha Chama kisera na kuzidi kuwaletea Watanzania maendeleo katika nyanja mbalimbali kupambana na umasikini yalitolewa na katibu wa shina jipya la Luton aliyechaguliwa siku hiyo, Ndugu Abraham Sangiwa, na kuungwa mkono na wajumbe wote waliyohudhuria ufunguzi huo.


Viongozi waliochaguliwa ni:


Albert Ntmi - Mwenyekiti
Abraham Sangiwa - Katibu Mkuu
John Mbwete - Mjumbe
Sammy Martin - Mjumbe
Norman Wage - Mjumbe

Wakati huo huo, siku mbili zilizopita, nikielekea kilele cha Mlima Kilimanjaro, katika kambi ya Barafu, ambayo ni kituo cha mwisho kabla ya safari ya kufika kilele cha Uhuru niliona bendera ya CHADEMA ikipepea.


Kwa mujibu wa taarifa nilizopata toka kwa wapagazi wanaosindikiza wageni kupanda Mlima Kilimanjaro wanaojulikana miongoni mwao kama "wagumu", kutokana na kazi ngumu wanayofanya kusindikiza wageni juu ya mlima huu maarufu, shughuli za CHADEMA zimeanza juu ya Mlima Kilimanjaro miaka mitatu iliyopita.

CHADEMA hawana tawi juu ya Mlima Kilimanjaro ila nilichoshuhudia mimi na jitihada za wana-CHADEMA kupeperusha bendera ya chama chao kwenye sehemu iliyo juu kuliko zote Tanzania. Kambi ya Barafu ipo urefu wa mita 4,600 juu ya usawa wa bahari.

Sunday, December 5, 2010

Jaffar Amin amewasili Moshi kupanda Mlima Kilimanjaro

Bwana Jaffar Amin amewasili Moshi leo mchana tayari kwa kushiriki nami kupanda Mlima Kilimanjaro kwa madhumuni ya kuchangisha pesa za hisani kwa ajili ya Sekondari ya Wasichana ya Chief Wanzagi ya mkoani Mara, pamoja na kuchangia asasi ya mjini Buoka inayoitwa BUDAP inayojishughulisha na miradi ya kusaidia walemavu kwa njia ya mafunzo na ajira.
Jaffar Amin, pichani, mara baada ya kuwasili Moshi mjini leo mchana, akiwa na hamasa kubwa ya kupambana na Mlima Kilimanjaro ambao unaonekana nyuma yake.
Baada ya kumpokea katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro, Jaffar alisema amejitayarisha vyema kupanda Mlima Kilimanjaro kuanzia Jumanne, 7 Desemba 2010 kwa muda wa siku nane.

Ni mara yangu ya tatu kupanda huo mlima, na mara ya kwanza kwa Jaffar. Matarajio na maombi kwa wadau mbalimbali ni kuchangia mojawapo ya walengwa wa tukio hili ambalo linajulikana kama The Mwalimu Nyerere/Mt. Kilimanjaro Charity Climb 2010.

Tafadhali changia mojawapo ya hawa wafuatao (au wote):

Jina la Akaunti:
Chief Edward Wanzagi Girls' Secondary School Fundraising

Benki:
National Bank of Commerce, Tawi la Musoma

Namba ya Akaunti:
030201191529

Pamoja na:

Jina la Akaunti:
Budap

Benki:
National Bank of Commerce, Tawi la Bukoba

Namba ya Akaunti:
027201092625
##################################

Saturday, December 4, 2010

Hardmad amerudi tea ulingoni

Baadaya ya kimya kirefu na kujifua kisawasawa, Hardmad amerudi tena kwa kishindo. Na safari hii amekuja na albamu inayokwenda kwa jina Imebaki Story ambayo ina jumla ya nyimbo 11.

zilizorekodiwa katika studio za 41 Records, Tatoo Records, na Maisha Studios za Dar es Salaam, na Click Studio ya Copenhagen, Denmark.

Usanifu umefanywa katika Studio za C4 nchini Denmark. Kwa kipindi cha mwezi mmoja Hardman alikuwa amejichimbia kambini kwa ajili ya mazoezi kwa kushirikiana na Kaka Zao Band atakayokuwa akifanya nayo maonyesho.

Picha na habari kutoka kwa Kwame Mchauru wa Maisha Music.