Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Tuesday, December 27, 2011

Maoni ya Amani Millanga kuhusu mafuriko ya Dar: sehemu kwa kwanza kati ya nne

Waathirika wa mafuriko wahame: sehemy ya kwanza kati ya nne
Na Amani Millanga

Ndugu zangu Watanzania, naungana nanyi kutoa mkono wa pole kwa waathirika wote wa mafuriko. Poleni sana kwa kupoteza ndugu, jamaa, na marafiki waliofariki katika mafuriko haya. Pia poleni sana kwa kupoteza mali zenu na vitu vyenu vyote kama nyaraka za umiliki wa nyumba zenu, vtambulisho na hata picha za familia n.k. ambavyo ni sehemu ya historia ya maisha yenu. Poleni sana na inshaallah Mungu atawasaidia. Anauona unyonge wenu. Auona umaskini wenu. Anauona udhalili wenu. Na kubwa zaidi Mungu muumba anauthamini sana utu wenu enyi waja wake mlioathirika na mafuriko. Naamuomba Mola Karima aziweke roho za marehemu pema peponi, inshallah. Nazipongeza jitihada zilizofanywa na watu binafsi, mwashirika binafsi pamoja na serikali za kutoa msaada wa kila hali na mali katika kuwafariji waathirika. Inshallah Mungu atakulipeni kwa sadaka zenu.

Wahame Mara Ngapi?
Haya si mafuriko ya kwanza kwa jiji la Dar es Salaam lakini n mafuriko ya kwaanza kufanya uharibifu mkubwa kama tulivyoshuhudia. Mafuriko yamefika hadi Ikulu, ofisi za UN na UNDP. Athari za mafuriko haya zimesababisha kuwepo kwa hoja nyingi kuhusiana na waathirika. Hoja inayotawala sana kwa baadhi ya watu na vyombo vya habari ni ile inayosema "waathirika wahame". Hoja hii haina mantiki wala mashiko yoyote. Hivi kweli hatuoni kwamba tayari waathirika wamekwishahamishwa na mafuriko? Hawako tena majumbani mwao. wanalala nje. Hivi tunataka wahame mara ngapi ili hali mvua imeishawahamisha? Kwa kweli hoja hii ya "wahame" tumeitoa katika wakati usiofaa kabisa. Huu si wakati wa kuwalaumu na kuwatia hofu ya kuwahamisha waathirika. Huu ni wakato wa maombolezo, huruma na huduma. Waathirika wanawalilia watoto zao, ndugu zao na jamaa zao waliofariki. wanalilia mali zao na historia yao. Kusema "wahame" si uungwana na si utu. Tukumbuke kwamba waathirika hawakuomba mafuriko. Lakini nitaitumia hoja hii ya "wahame" katika makala haya kutoa mchango wangu wa nini kifanyike katika wakati huu mgumu kwa taifa ambalo limesherehekea miaka 50 ya uhuru wake hivi karibuni.

Hoja za msingi kwa wakati huu: ni namna gani waathirika wanapata chakula na maji safi na salama; ni namna gani waathirika wanapata vyoo na bafu; ni namna gani waathirika wanalala; na ni namna gani waathirika wanapata nguo za kujisitiri; na tumejipanga vipi kuwakinga waathririka na magonjwa ya kuambukiza ya kipindupindu, malaria, kuhara, minyoo, n.k. Haya ndiyo mambo muhimu ya kufanywa kwanza. Ingawa baadhi yanafanyika basi tuongeze juhudi zaidi ya kutoa huduma zaidi. Pili, ni suala la wapi wanahamia waathirika hawa baada ya Mchikichini. Suala hili linaibua maswali mengi, lakini baadhi yake ni: Je, wahamishiwe wapi? Je, tumeishayatenga au kuyapima maeneo hayo ya kuwahamishia waathirika? Je, tutawalipa fidia za nyumba na ardhi yao? Je, fidia hiyo itachukua muda gani kumfikia muathirika? Je, wwanza kuhamishwa huko kwenye maeneo mapya lini? Maswali ni mengi yanayohusu huduma za afya, elimu na jamii huko wanakohamishiwa maana watu takribani 5,000 si wachache.

Itaendelea.

No comments: