Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Tuesday, August 28, 2012

Hatimaye, watu wa sensa hawa hapa

Jumapili, tarehe 26 Agosti, nilikaa nyumbani siku nzima nikisubiri kuhesabiwa kwenye Sensa ya Taifa lakini sikuona mtu hata mmoja kuja kuniuliza swali. Hatimaye leo maafisa wa sensa ya Taifa wamefika kunihoji maswali yao 62, ambayo kila mshiriki anapaswa kuyajibu.

Wengi wetu hatukukumbuka kuwa ni zoezi la juma zima.
Mimi, kushoto, nikijibu maswali ya Sensa ya Taifa leo asubuhi. 
Ndani ya muda wa dakika kumi zoezi lilimalizika na wakaondoka.

Pamoja na kwamba wengine tulikuwa na shauku kubwa ya kukamilisha kazi hii kuna Watanznia wenzetu ambao kabla ya zoezi hili kuanza wamekuwa wakiendesha kampeni ya wazi kuhimiza Waislamu wasishiriki kwenye sensa kwa sababu maswali yale 62 hayaulizi dini ya anayehesabiwa.

Nimejaribu kuuliza hili swali lakini mpaka leo sijasikia jibu lake: tunataka kujua kuna Watanzania wangapi wa dini mbalimbali ili tutumie hizo takwimu kufanya nini? Mwenye jibu naomba anifahamishe.

No comments: