Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Tuesday, May 21, 2013

Nkrumah bado anakumbukwa


Mwaka 2008 mimi na baadhi ya wadau kutoka nchi wanachama za Jumuia ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) tulialikwa nchini Zimbabwe kuandika kuhusu uchaguzi mkuu wa nchi hiyo.

Baada ya kura kupigwa tulitembelea kituo kikuu cha kutoa taarifa za uchaguzi cha Tume ya Uchaguzi ya Zimbabwe (ZEC) jijini Harare ili kupokea taarifa zilizoendelea kufika hapo toka sehemu mbalimbali za Zimbabwe.
Maafisa wa Tume ya Uchaguzi wa Zimbabwe wakitangaza matokeo ya uchaguzi wa Zimbabwe.
Wadau ambao walikuwa waandishi wa habari walikuwa ni pamoja na Bayano Valy kutoka  Msumbiji (aliyesimama, kushoto), na Penny Kamanga (aliyesimama, kulia) kutoka Malawi.
Nimewahi kuandika kwenye blogu yangu ya Kiingereza kuhusu tofauti za kimtazamo kati ya Dk. Kwame Nkrumah, na Mwalimu Julius Nyerere. Kwenye picha ya hapo juu, nukuu iliyopo kwenye fulana aliyovaa huyo mwanahabari aliyekaa kulia inatanabahisha kufanana kwa baadhi ya mitazamo yao. Tafsiri ya nukuu:

Uhuru wa Ghana hauna maana iwapo hautahusishwa na ukombozi kamili wa Afrika.

Ni msimamo ambao Mwalimu Nyerere naye alikuwa nao. Wakati wa uongozi wake, Tanzania ilitoa msaada mkubwa wa hali na mali kuunga mkono vyama vya ukombozi kutoka nchi za Kiafrika ambazo zilibaki chini ya utawala wa kikoloni na kibaguzi, ikiwa ni pamoja na Msumbiji, Zimbabwe, Afrika Kusini, na Namibia.

No comments: