Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Friday, June 7, 2013

Lugha yetu Kiswahili: Ulemavu wa ngozi?

Imezuka desturi ya miaka ya hivi karibuni ya kubadilisha baadhi ya matumizi ya lugha na kutunga matumizi ambayo yanakuwa mbadala ya mazoea yaliyopo. Mojawapo wa mabadiliko ya lugha ya aina hii ni kuacha kutumia neno "zeruzeru" na badala yake kutumia "mlemavu wa ngozi."

Mabadiliko haya yanaiga desturi iliyoanzia Marekani ya kuacha kutumia maneno, misemo, au majina ambayo matumizi yake yalionekana kudhalilisha au kuudhi makundi kadhaa ya jamii ambayo yalibaguliwa kwa njia tofauti, ikiwa ni pamoja na jinsia, dini, rangi ya ngozi, na kadhalika.

Mathalani, kwa mantiki hiyo, baadhi ya Wamarekani hutumia physically challenged (mwenye changamoto za kimaumbile) badala ya maneno invalid (asiyejiweza), handicapped (kilema), au disabled (mlemavu).

Mimi naafiki ubunifu wa misemo mipya mbadala na kuacha matumizi ya misemo ambayo inadhalilisha. Lakini bado sijaona mantiki ya matumizi ya "mlemavu wa ngozi" badala ya "zeruzeru." Kamusi ya Kiswahili Sanifu (Oxford, toleo la pili 2004) inaeleza zeruzeru kuwa ni "...mtu ambaye nywele na ngozi yake imekosa rangi yake kamili na badala yake kuwa nyeupe sana na ambaye macho yake hayawezi kuvumilia mwangaza mwingi; albino."

Haya maelezo yanadhalilisha?

No comments: