Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Saturday, June 29, 2013

Ziara ya Rais Barack Obama Tanzania: yale yale!

Kama nilivyoandika kwenye blogu hii hivi karibuni, ziara ya rais wa marekani nchini Tanzania huwa inakuja na usumbufu wa kiwango cha juu kwa raia.

Kuna taarifa kuwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere utafungwa kwa vipindi virefu tarehe 1 na 2 Julai 2013, siku ambazo Rais Barack Obama atakuwa ziarani Tanzania. Sehemu ya taarifa niliyoiona inasema:
Please be advised due to VVIP movement (US Presidential delegation) scheduled visit to DAR on 1st July, JNIA will be closed as per below:
 Monday 1st July from 02:20 to 03:25 pm
Tuesday 2nd July from 10:40 to 11:45 am
 Kindly ensure your travel arrangements are in order to avoid any disruption to your trip.
Taarifa inaeleza kuwa tarehe 1 Julai, uwanja utafungwa kati ya saa 8:20 usiku wa manane mpaka saa 9:25 alasiri na tarehe 2 Julai uwanja utafungwa saa 4:40 hadi saa 5:45 asubuhi.

Mimi nilipendekeza kupunguza usumbufu kwa raia huyu mgeni mashuhuri angefanyia mazungumzo yake na wenyeji wake Butiama. Ziara hii Dar es Salaam inasumbua watu zaidi ya milioni nne; Butiama itasumbua watu kama 20,000 tu. Lakini nani atanisikiliza?

No comments: