Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Sunday, July 28, 2013

Maendeleo (na makelele) yameingia Butiama

Butiama bado ni wilaya changa kabisa, lakini tayari mabadiliko yatokanayo na miji (na kero zake) yameanza kuonekana Butiama.

Makelele ni mojawapo ya kero za miji ambayo sehemu kama Butiama haikuwa nayo mpaka hivi karibuni. Butiama haikuwa na huduma ya basi linalosafiri moja kwa moja kwenda Mwanza na hapo awali wasafiri walilazimika kusafiri mpaka njia kuu iendayo Mwanza, sehemu iitwayo Nyamisisi, au kuanzia safari Musoma. Miaka michache iliyopita huduma ya basi la moja kwa moja kutoka Butiama hadi Mwanza ilianzishwa na kuleta kero ninazozungumzia.
Basi la kuelekea Mwanza kwenye stendi ya Butiama.
Basi hilo linapoegeshwa alfajiri kusubiri abiria ni kawaida ya madereva wake kupiga honi mfululizo kwa muda mrefu na kusababisha makelele kwenye eneo kubwa la Butiama. Butiama ni kijiji kidogo kwa hiyo mfululizo wa honi hizo za kila kukicha ni usumbufu mkubwa kwa wakazi wengi wa Butiama.

Sijaelewa mantiki ya kupiga hizo honi ingawa naamini zinakusudiwa kuwaamsha abiria wanaosafiri.Lakini ni vigumu kuelewa utaratibu wa abiria anaekusudia kwenda Mwanza kutegemea kuamshwa na honi ya basi.

No comments: