Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Sunday, July 13, 2014

Wakati mwingine picha zinadanganya

Hii (chini) ni picha ya eneo la Dar es Salaam, katika makutano ya barabara ya Bibi Titi na Mtaa wa Zanaki, ambalo kwa miaka mingi nimekuwa napita kwa mguu na ni eneo ambalo limebadilika sana katika kipindi hicho cha karibia miaka 30. 

Kushoto mwa picha hii (hapaonekani) kuna jengo kubwa lenye ofisi na maduka kwenye ghorofa za chini na nyumba za kuishi kwenye ghorofa za juu. Ni sehemu ambayo zamani waliishi Watanzania wa jamii ya Kiasia . Jengo lililojengwa hapo lilibadilisha kabisa taswira ya eneo hilo na liliongeza idadi ya majengo mapya ambayo yanachipuka Dar es Salaam kila kukicha. Majengo mengi ya zamani na ya kihistoria yanaendelea kubomolewa.


Lakini pamoja na mabadiliko makubwa yanayoendelea kutokea kwenye baadhi ya maeneo ya Dar es Salaam ninahisi kuwa picha hii haiakisi ukweli wa hali ilivyo katika eneo hilo. Ukweli ni kuwa picha hii inapamba zaidi hali halisi.

Nimeshapita kwenye eneo hili mara mia kadhaa lakini sijaona hali hiyo nzuri ambayo naiona kwenye picha hii. Kwa hakika teknolojia ya kamera imefanikiwa kupamba ukweli kwa sifa bandia.

No comments: