Kushoto mwa picha hii (hapaonekani) kuna jengo kubwa lenye ofisi na maduka kwenye ghorofa za chini na nyumba za kuishi kwenye ghorofa za juu. Ni sehemu ambayo zamani waliishi Watanzania wa jamii ya Kiasia . Jengo lililojengwa hapo lilibadilisha kabisa taswira ya eneo hilo na liliongeza idadi ya majengo mapya ambayo yanachipuka Dar es Salaam kila kukicha. Majengo mengi ya zamani na ya kihistoria yanaendelea kubomolewa.
Lakini pamoja na mabadiliko makubwa yanayoendelea kutokea kwenye baadhi ya maeneo ya Dar es Salaam ninahisi kuwa picha hii haiakisi ukweli wa hali ilivyo katika eneo hilo. Ukweli ni kuwa picha hii inapamba zaidi hali halisi.
Nimeshapita kwenye eneo hili mara mia kadhaa lakini sijaona hali hiyo nzuri ambayo naiona kwenye picha hii. Kwa hakika teknolojia ya kamera imefanikiwa kupamba ukweli kwa sifa bandia.
No comments:
Post a Comment