Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Sunday, October 31, 2010

Wakala wa CCM kituo cha hospitali ya Butiama yuko ngangari

Nilivyotembelea kituo cha kupiga kura cha Hospitali ya Butiama leo asubuhi nilibaini mtu mmoja amekaa pembezoni, akiwa anaangalia kwa makini mienendo ya kila mmoja pale kituoni. Mwanzo nilifikiri labda ni afisa wa Usalama wa Taifa.
Wakala wa CCM kushoto, akinitupia jicho nilipopiga picha hii leo asubuhi kwenye kituo cha kupigia kura cha Hospitali ya Butiama.
Nilipata ujasiri wa kumuuliza yeye ni nani na akaniambia kuwa ni wakala wa Chama cha Mapinduzi (CCM). Sijashangaa kuwa hakuwepo wakala wa chama kingine kwa sababu mbili: Kwanza, mbunge wa CCM wa jimbo la Musoma Mjini, Nimrod Mkono, amepita bila kupingwa; na pili, nguvu ya upinzani, hata kwenye ngazi ya udiwani, siyo kubwa sana.

Kwenye chaguzi za serikali za mitaa, ni mgombea wa CCM ndiyo aliyeibuka mshindi na kuchaguliwa kuwa mwenyekiti wa kijiji.

No comments: