Tembelea Butiama

Tembelea Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Karibu Butiama / Welcome to Butiama

Kurasa Muhimu

Thursday, June 14, 2012

Francis Cheka kupambana na Joseph Kaseba siku ya Saba Saba

Bingwa wa IBF wa Afrika wa uzito wa Super Middleweight, Francis Cheka, ataingia ulingoni tarehe 7 Julai 2012 kupambana na Joseph Kaseba katika pambano linaloandaliwa na Global na kuratibiwa na Kaike
Francis Cheka, kushoto, na Joseph Kaseba, kulia.
Siraju.

Cheka alitwaa ubingwa wa mabara wa IBF afrika alipomshinda Mada Maugo katika pambano liliofanyika ukumbi wa PTA Dar es Salaam tarehe 28 Aprili 2012.

Pambano hilo litakuwa pambano la kwanza kufanyika katika uwanja mpya wa Taifa wa Dar es Salaam. Baadhi ya mapambano yatakayosindikiza pambano hilo ni pamoja na Adiphoce Mchumia dhidi ya Ramadhani Kido, Amos Mwamakula dhidi ya Rashini Ali, Mkongo Kanda Kabongo dhidi ya  Said Mbelwa, na bondia chipukizi Ibrahimu Class toka kambi ya masumbwi Ilala inayonolewa na kocha Habibi Kinyogoli atapambana na Sadiki Momba.

Picha na habari kwa hisani ya superdboxingcoach.

No comments: